May 15, 2011

HEKO SIKU YANGU YA KUZALIWA

Nipo kimya kwelikweli, lakini naamini ipo siku nitaeeleweka vema kwani juhudi hizi si bure kuna mahali nahitaji kuelekea. Najua nimekosekana hapa lakini naamini ninyi wanablogu ni watu wa kwanza mnaotakiwa kunielewa kuliko viumbe wengine. Kuna Yasinta,Koero,Mkodo,Mtanga,Kaluse,Kamala,Mbele, mzee wa Livet, Erick,Camilla na wengineo hakika nipo nanyi ila nipo gereza la harakati kila saa. NAJIPONGEZA MWENYEWE KWENYE HII SIKU YANGU YA KUZALIWA MAANA RAHA JIPE MWENYEWE.

PAMOJA NA HILO
Rafiki yangu huyu hapa chini amekuwa mtu muhimu sana, naamini ni vema kumtunukia nishanio ya heshima kwamba nakuthamini sana rafiki yangu na dada yangu pia ndugu yangu. Najua wajua kile nikifanyacho kwani siku si nyingi naweza kutoka kwenye gereza hili na kurudi kwa kasi kwenye blogu ya wanakijiji wa Lundu kule nyasa.
Asante dada Yasinta a.k.a Kapulya.

7 comments:

  1. Mwenyezi Mungu na akulinde uwe na amani siku zote na akupe nguvu kwa yote unayofanya. Na katika siku yako hii ya kuzaliwe pia akuonyeshe mwanga wa maisha. Na akupe nguvu kuona uyafanyayo mafanikio yake yatakuwa MAZURI. UWE NA SIKU NJEMA MARKUS...NIWONA LELU GWALI NA SOMBA YATI KULYELYEKA KWELI....NENE NIGANA LEPI MAKEKI AGA...MBWITU:-)

    ReplyDelete
  2. Hongera sana mkuu Markus..uzidi kukata miaka na kuzidi kupata mafanikio, hata wengine waweze kunufaika nayo.Uwe na siku njema!

    ReplyDelete
  3. Hongera mkuu, wahenga husema `kimya kingi kina mshindo...' au sio vyovyote iwavyo twakutakia mafanikio mema, na `happy birthday yako mkuu' TUPO PAMOJA

    ReplyDelete
  4. Samahani, nje ya mada kidogo:

    Hebu pita hapa: http://changamotoyetu.blogspot.com/2011/05/majibu-ya-mmiliki-wa-tuzo-za-blog.htm

    Au pia hata hapa:http://kamalaluta.blogspot.com/2011/05/wanaotoa-tunzo-za-bloggers-na-watoe-kwa.html

    Na usiishie hapo kuna hapa pia: http://mtayarishaji.blogspot.com/2011/05/majibu-ya-mmiliki-wa-tuzo-za-blog.html

    Mwisho pia kuna hapa: http://bwaya.blogspot.com/2011/05/wanablogu-wanasemaje-kuhusu-utaratibu.html

    NINA UHAKIKA HAUTAKOSA LA KUSEMA KULINGANA NA UTAKAVYOLITAZAMA JAMBO LENYEWE.

    ReplyDelete
  5. Kila la kheri Mkuu! Tuko Pamoja!

    ReplyDelete
  6. Hongera sana twakutakia maisha marefu, furaha tele na afya njema

    ReplyDelete
  7. Anonymous03 June, 2011

    HAYA YAMENIPITAJE? MIMI NI MSOMAJI MZURI TU WA BLOG.. NIMEKUWA NIKIPITIA BLOG MBALIMBALI LAKINI HII SIKUWAHI KUKUTANA NAYO... SIJAPATA KUCHIMBA AU KUSOMA BACKGROUND I MEAN NINI HAS LENGO KUU LA BLOG HII YA KIKWETKWETU....BWANA MPANGALA ANATAKA KUWAELEZA WATU KUHUSIANA NA NINI HASA? JUST CURIOUS ILI NAMI NIWE MDAU 'ACTIVE'- HAPPY BELATED BIRTHDAYMPANGALA!!! D NDUNGURU. MIKOCHENI, DSM.

    ReplyDelete

Maoni yako