December 02, 2012

TAARIFA KWA WAWEKEZAJI WAPYA KATIKA KILIMO CHA MITI YA MBAO, KARATASI NA NGUZO.

Fresh Farms & Tours (T), biashara tanzu ya Anesa Co.,Ltd (Nyaluke Business Empire); inayojishughulisha na upandaji, utunzaji na uendelezaji wa mashamba ya miti ya mbao, karatasi na nguzo-mkoani Iringa. Pia inahusika na uvunaji na usambazaji wa mazao ya miti, (mbao na nguzo za umeme) sambamba na ufugaji.
Fresh Farms ilianzisha programu maalumu, mapema mwaka jana; inayolenga kuwawezesha watanzania wengine kuwekeza katika kilimo cha miti kwa urahisi. Tayari makumi wa watanzania wamechangamkia fursa hii. Fresh Farms & Tours (T) tunapenda kuwaarifu wale wote wenye nia ya kuwekeza nasi; KWAMBA kuanzia tar 1, Feb, 2013 kutakuwa na mabadiliko ya bei na gharama za uendeshaji kwa mashamba ya miti. Mashamba tunayoyauza laki sita kwa sasa; bei mpya itakuwa milioni moja; na yale tunayouza laki nane gharama yake itakuwa milioni moja na nusu.
Bei hizi hazitawaathiri wateja wa awali na wale ambao wamekwisha wasilisha oda zao. Fresh Farms & Tours (T) tunaendelea kuboresha huduma, taarifa na usaidizi kwa wote wanaowekeza nasi. Kabla ya mwisho wa mwaka huu; tutazindua tovuti maalaumu itakayobeba taarifa za uwekezaji katika kilimo na ufugaji; pia kila anaewekeza nasi atapata nafasi ya kufungua akaunti yake katika tovuti hiyo; na akaunti hiyo itamwezesha kufuatilia mwenendo wa mashamba yake popote alipo duniani. Fresh Farms & Tours (T)-GREENING THE WORLD AND FEEDING PEOPLE. (C) Anesa Co., Ltd

No comments:

Post a Comment

Maoni yako