January 21, 2013

MRADI WA MAJI SAFI NA SALAMA KIGONSERA-MBINGA

Na Mwandishi Wetu, Kigonsera

Kigonsera ni miongoni mwa miji muhimu sana wilaya ya Mbinga. lkaini kwa kipindi kirefu baadhi ya wakazi wa mji huo walikuwa wakikabiliwa na uhaba wa maji safi na salama. kwa sasa mradi mkubwa wa kusambaza maji safi na salama katika wilaya ya Mbinga umeshika kasi huku mji wa Kigonsera ukiwa miongoni mwa miji muhimu sana kiuchumi na biashara.
 Ni mji ambao upo pembezoni mwa barabara kuu iendayo Songea mjini kutokea Mbinga. Kutokana na shughuli nyingi za kiuchumi, watu wengi hutumia mji huu kufanya biashara na zingine za ujenzi wa taifa, hivyo wanahitaji huduma muhimu sana ili kusogeza mbele maendeleo ya mji wao na taifa kwa ujumla.
       
Pichani msimami wa Mradi ndugu Egbart Jeremy akiwa katika intake ya maji safi na salama mjini Kigonsera, ikiwa ni moja ya miji ambayo inatakiwa kufanyiwa marekebisho ya kuleta uhuduma ya maji kwa wakazi wake.


     
Wahandisi wa maji wa wizara ya maji, mkoa wa Ruvuma na wilaya ya Mbinga wakikagua ujenzi wa tanki la maji lenye uwezo wa kubeba ujazo wa mita za ujazo mia mbili(200) katika mji wa Kigonsera. Tanki hilo lipo katika ujenzi na kampuni ya ujenzi ya Mwalongo Cont ya mkoani Njombe.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako