February 07, 2013

MVUA KUBWA YANG'OA MADARAJA BARABARA YA LITUHI-MBAMBA BAY


Na Egbart Jeremy, Nyasa

Mvua mkubwa iliyonyesha mapema mwezi huu imesababisha baadhi ya miundombinu kuharibiwa. Miongoni mwa maeneo yaliyoharibiwa kabisa ni Daraja la Mbaha, na barabaraba ya Lituhi kwenda Mbamba kwa ujumla, ambapo imejifunga kutokana na kukosekana kwa vivuko vingine. 
Moja ya maeneo yaliyoharibiwa kutokana na mvua kubwa iliyonyesha wilayani Nyasa
Mvua hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa ukosefu wa mawasiliano baadhi ya vijiji hadi vijiji katika mwambao wa ziwa Nyasa. Sio madaraja pekee, bali ukuna uharibifu mkubwa sana vyanzo vya miradi ya maji hususani katika kijiji cha Lundu. 
Hadi sasa hali haijatengemaa kiasi amabcho wakazi wa maeneo yaliyokumbwa na uharifu wanakosa huduma muhimu kutokana na ukosefu wa usafiri kutoka eneo moja kwenda jingine. Ikumbukwe miradi ya maji katika kijiji cha Lundu ni moja ya miradi mipya iliyokamilishwa mapema mwishoni mwa mwaka jana hivyo kuleta nafuu kwa wakazi wake. Lakini kutokana na uharibifu uliotokana na mvua kubwa kunyesha utalazimisha miradi hiyo kuanza kukarabatiwa upya.

1 comment:

  1. mvua ni nzuri lakini ikitokea hivi kwa kweli inakuwa tatizo kubwa sana kwa jamii.

    ReplyDelete

Maoni yako