March 11, 2013

MAONI YANGU KATIKA MIJADALA YA UHURU KENYATTA VS RAILA ODINGA, SHUKRANI KWA BEN SAANANE KUIBUA HOJA MUHIMU NA NYETI


Nakiri moja ya upumbavu mkubwa ni Barrack Obama kuwa kikaragosi kwake na serikali. Mwanzoni kupitia Hilary Clinton walisema wakenya wasichague watuhumiwa wa ICC yaani Kenyatta na Ruto. Baadaye akaja Barrack Obama akasema atawaunga mkono wakenya katika chaguo lao. UNAFIKI, na nilishawaambia watu Barrack Obama sio mwafrika kwa vile tunavyotaka kumtafsiri kama akina Jesse Owen, Jesse Jackson ambao ni zao la utumwa.

Obama hakuachagua lakini yeye sio zao la utumwa bali mapenzi tu wa binti na mvulana. hajui madhira ya akina jese jackson. kwa suala la kenya Raila Odinga nampenda harakati zake lakini bado naguswa na UZEMBE aliofanya na kudhani atashinda kirahisi. Nimeandika hili, inshallah itachapishwa wiki ijayo jumanne(TAZAMA). Odinga amejitakia sana, kwa njia zake alizopita tangu 2002, 2007 na 2013 sishangai kushindwa kwake.

Hata wengi walipomshinikiza Jaji Willy mutunga katika kesi ya Uhuru kenyatta na Ruto kutogombea, jaji mutunga alisema wanaopinga hawana hoja. Kimsingi Odinga alikuwa na timu dhaifu mno, wala hata CHADEMA sijui kupeleka nini au nini sijui bado Odinga alikuwa na timu dhaifu sana kuliko ile ya mwaka 2007 iliyojaa wababe wa siasa na wenye ushawishi. Hivi nani pale alikuwa na msaada kwa Odinga mwaka huu?

Sioni hata mmoja. Kwahiyo kuwalazimisha wakenya wamchague Odinga ni ukosefu wa heshima tu. wakenya sio wajinga, na wanaolalamika ni watu wa Kisumu tu. Ujinga aliofanya Odinga ahata akiongea na mimi nitamwambia ulifanya makosa haya na haya. kwahiyo CHADEMA kumsaidia Odinga ni kawaida na tunawaheshimu kwa hilo, lakini uamuzi wa mwisho ulikuwa mikoni mwa wakenya.

Sio Obama ambaye sio raia wa kenya. ....... sio mpiga kura wa kenya. kama alitaka Odinga ashinde alipaswa kuwa na adabu sasa. Marekani kutomtaja sio issue kabisa, haitabadilisha kitu, ni ujuha tu. wala Marekani ikitaja jina la kenyatta haina maana ndio inahalalisha. Marekani sio wakenya. 

Hayo mataifa yaliyowapongeza WAKENYA, na WAKENYA wamemchagua nani? Je, kupingwa matokeo mahakamani kunazuia kupongezwa kwa Uhuru Kenyatta ambaye ametangazwa na TUME? ....
na kama Raila Odinga akishinda hiyo kesi, kuna sheria inayozuia kutompongeza Raila Odinga? mimi nadhani USA kutotaja jina la kenyatta ni woga na udhaifu kiakili, sababu ilibidi hata pongezi wasitoe wasubiri hatima ya majibu ya mahakama. ... vilevile, mataifa ya magharibi kutotaja jina kenyatta au kutompongeza bado hakumanishi wao wana uhalali wa kuwamrisha wakenya wamchague nani. .....kwa upande mwingine kisiasa Odinga amejitakia ANGUKO.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako