April 03, 2013

GHASIA ZA TUNDUMA, HALI SIO NZURI SANA


Ghasia zinazoendelea katika mji wa Tunduma ulioko mkoani  Mbeya zimechochea uharibifu kijamii. Tunduma haiko katika hali nzuri.

Vurugu kama hizo ziliwahi kutokea mjini Mwanza na kuhusisha wamumini wa imani ya kikristo na Kiislamu. Mauaji yalitokea na serikali ilifanya juhudi kuwakamata wahusika.  

Hapa mwakilishi wa Blogu ya Lundunyasa, anaelezea kwa ufupi sana juu ya kile kinachoendelea mjini humo.

Ni kwamba inaelekea hotuba ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu uchinjaji bado haijaeleweka, hivyo wakristo bado walikuwa na msuguano na wenzao juu ya nani achinje. 
Tamko la Polisi lilisema waislamu waendelee kuchinja sasa leo alfajiri vijana wa kikristo walienda machinjoni na kumgawia kichapo cha kutosha mchinjajiwa kiislam ambaye alifanikiwa kutoroka. 

Baada ya hapo wakristo nasikia ndiyo wakaanza hizo fujo ikiwemo pamoja na kufunga barabara, kuharibu msikiti, kubomoa nyumba ya polisi mmoja aliyejenga uraiani, wameandamana na biblia mikononi kudai haki ya kuchinja. 

Polisi wa Tunduma kazi imewaelemea na ikabidi nguvu itoke mkoani na RPC yupo huko sasa hivi. Juzi kanisani Padre mmoja alitoa kauli kuwa kama hawa watu wanataka kuchinja basi watuchinjie na kitimoto.

Kisa kikuu ni kwamba madalali wa mifugo wamegoma kupima nyama zinazochinjwa na wakristo, hivyo wakristo wanahoji kwanini iwe hivyo. Pia mtaani mabucha ya nyama zilizochinjwa na waislamu zimeganda hakuna wanunuzi.

Raia ilibidi wakimbilie mahakamani kwa kuona kwamba ndiyo sehemu pekee ya usalama kwao, hivyo ikalazimu mahakama kuhairishwa ili kuepusha balaa. Kale kamchezo kakuchoma matairi na kufunga barabara kakawa ndiyo mchezo wa kawaida.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako