December 09, 2017

SALAMU KUTOKA LUNDU, ZIWA NYASA

Nipo kijijini kwetu Lundu kwa muda wa mwezi mmoja sasa. Naendelea kukusanya taarifa mbalimbali zinazofaa kuchapishwa hapa barazani “Karibuni Nyasa”.  Kama tunavyoona habari mbalimbali za utalii, basi ndivyo utakavyosikia habari usizowahi kuzijua kutoka mwambao wa Ziwa Nyasa. Mazingira yanayovutia mno, yenye kuhitaji kutembelewa.
 
Kuna picha mbili; ya kwanza nikiwa katika Mto Chipapa, uliopo mtaa wa Likwambe hapa hapa kijijini Lundu. Ni mto ambao miaka 1990 ulikuwa ukitiririsha maji yake mwaka mzima kwa ufasaha. Lakini sasa mambo yamebadiliika, hakuna uwezekano huo. Kwahiyo mto huo unangojea msimu wa masika kama hivi sasa uweze kuwa na maji ya kutiririsha hadi Ziwa Nyasa.


Safari yangu katika eneo hilo lilikuwa kufuatilia uchomaji wa Mkaa, ambao haujawahi kufanyika hapa kwetu Lundu. Nyaka hizi maisha yamebadilika, watu wanahitaji zaidi mkaa, majiko ya mkaa na unga wa sembe kwaajili ya chakula. Utegemezi wa unga wa Muhogo umepungua.

Picha ya pili nikiwa na wanafunzi wa Shule ya Msingi Lundu. Wanafunzi wanaoonyesha uchu wa kutafuta maarifa ingawa mazingira yamekuwa yakiwabana kidogo. Kwa hayo machache nawatakieni maandalizi mema ya Noeli na mwaka mpya.

Kizito Mpangala

Lundu, Nyasa

12 desemba, 2017.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako