June 04, 2008

Tazama Uzuri wa Nyasa Yetu, Mazingira yetu

Nilipoandika kwamba mazingira safi,kama mlidhani nacheza basi mmenoa.Nyasa ndiyo jioni hapo uzuri unajionyesha wenyewe.Kwa mara ya kwanza nilipoitazama picha hii nikajiuliza swali moja.Kwanini yule rafiki yangu Christine wa Bavaria alilia na kugomea kuondoka Lundu pale ufukweni?Lakini nilipata swali la pili,kwanini wazazi wake waliamua kuwapo pale kwa masaa matano?,Sasa majibu nayapata kwamba ile kauli ya rafiki yangu yule kwamba "hapa naona nimependa upendo wangu wote,natamani ningelikuwapo kila siku,hakuna baridi kama kwetu,joto siyo kali ni la wastani haliumizi.Mbona hamchangamkii hii hali?lakini kifupi ni eneo zuri,nakuahidi Markus nitafika peke yangu mara nyingine bila hawa wazazi ambao wananilinda kama mtuhumiwa".Sikuwa na majibu ya haraka,na ingawa hajafika tangu mwaka 2003 lakini nimeamua kweka mtandaoni utamu wa nyasa kama huu,kwa yeyote ahayehusika karibuni nyasa

1 comment:

  1. Nitamuunga mkono huyo rafiki yako. Ila sasa mie nitajenga nyumba ili nisipate taabu kuamka na kukaa tu.

    ReplyDelete

Maoni yako