August 23, 2008

Haya tena kama kawaida wanyasa

najua wengine mmenuna eti kisa sijablogu kwa wiki kadhaa,jamani ni majukumu haya kuvua samaki kwahiyo tuliondoka kijijini kwetu kwenda vijiji vya mbali kuvua samaki kwahiyo hata muda wa kwenda mbinga mjini ikawa ngumu sanna.Eti leo hata dada Janeth kaandika ujumbewa hasirakwanini sijablogu na nimeweka picha zamani sana.Niliomba msamaha lakini inaonekana hana raha na kasi ya kublogu siku hizi.Haya kama kawaida wanyasa nipo tena. sijasahau kuna habari ya kutembea peku hebu isome hapo kaka Mbilinyi

3 comments:

  1. hata mimi nilikuwa najiuliza kama umeacha kublog au pole na majukumu. msaimie janeth

    ReplyDelete
  2. Kaka Mpangala,
    Najua wewe ni mtu wa kuchakarika sana na kwa kweli nakupongeza sana kwa kuwa sharp pia unafanya vizuri kutuambia nini kinaendelea.
    Mimi nilihisi umeenda Beijing China kuangalia nini kinaendelea ili 2012 London Olympic tufanye mambo kwani najua tutapata wawakilishi wa Ku Kayak kutoka Nyasa na kuogelea, Yaani tumeshindwa Tanzania nzima bara na visiwani mikoa yote 26 kupata mtu wa kutupa Jiwe (tufe) kurusha mkuki, kuruka long jump, hata kulenga shabaha, kukimbia? Je kaka Mpangala unakubali? kwa kuwa sasa unafanya mazoezi naamini 2012 watatukoma lazima turudi na medali za uhakika.

    ReplyDelete
  3. Yaani nimejikuta nachangayikiwa kidogo kwani mikoa 26 tumeshindwa halafu wale jamaa waliopo milioni 2 jamaika wameweza? nimekwisha kuanza mazoezi kwaajili ya olimpiki ijayo na nimekusanya vijana wenye kasi ya kuogelea we acha achana na yule jamaa kashinda medali nane za dhahabu yaani kwetu tunamwona kama mwigizaji Eddy Murphy au Ze Comedy wa hapa bongo yetu hasa yule anajiita Masanja Mkandamizaji na mwezie Joti

    ReplyDelete

Maoni yako