October 10, 2010

KAZI + SHULE= RATIBA NGUMU

Kwa kweli nimebanwa sina jinsi nalazimiika kukubali kwamba ratiba imekaa katika mantiki iliyopinda. Lakini jukumu hilo nitaliweza tu. Blogu ipo sana siyo lile wazo la mzee wa Nyegerage kwamba itakufa lini. Nipo sana waungwana

4 comments:

  1. Paroko, Mwanafalsafa na msomi ULIYEBOBEA unasoma nini tena? Au unatekeleza ule msemo wa elimu haina mwisho kwa vitendo?

    Hongera kwa kujiongezea maarifa zaidi, na kwa jinsi ninavyokufahamu hutaiachia blogu hii ife. Makala zako kwa kawaida ni pevu, dhati, korofishi, komavu na zenye kuchochea fikra. Tunategemea mavuno zaidi!!!

    ReplyDelete
  2. Ni furaha kusikia unachofanya. Ungesema unavua samaki nisingefurahia sana. Elimu ni msingi wa maisha na unajijengea msingi wa maisha yako na pia familia tarajiwa. Kublog kupo ila umemissiwa. Nakutakiwa kila la kheri!!

    ReplyDelete
  3. Kaka Matondo, hakika niseme sijawa aliyebobea, kwa kweli sijawa msomi zaidi kuwa mimi tu jabali a.k.a mwamba wa nyasa. laiti ningelikuwa kama wewe, kubobea katika lugha na mengineyo hakika ningelikuwa gwiji. laiti nginekuwa kama Mzee wa Mbele ningelisema na kujiona mjivuni. lakini hakika sijawa mjivuni bali ni kijana mtafutaji na mwenye UCHU wa kujua maana ukijua unajua tu. kaka Matondo nami nataka siku moja niwasimamie wanafunzi wa masters kama wewe unaonaje hili wazo?

    ReplyDelete

Maoni yako