October 16, 2012

FRESH FARMS(T) YATEMBELEWA NA MHADHIRI WA CHUO KIKUU CHA MOSHI

Siku tatu zilizopita; Fresh Farms (T) tulitembelewa na mgeni Mr. Emmanuel Lulandala ambaye ni mhadhiri wa chuo kikuu cha Ushirika Moshi. Tulimzungusha kwenye baadhi ya mashamba yetu ya miti ya mbao na karatasi na alijifunza mengi. Katika picha hii: tulikuwa katika bustani ya miche ya miti ya mbao na karatasi, ambayo tunatazamia kuipanda kwenye ekari mpya 340 kwenye msimu huu unaoanza Novemba. Kutoka kushoto: Emmanuel Lulandala, Katikati: Albert Nyaluke Sanga (C.E.O- Fresh Farms (T), Kulia: Jadili Kaguo (Farm Mager-Fresh Farms (T). Fresh Farms (T) ni biashara iliyopo chini ya NYALUKE GROUP LTD (Nyaluke Business Empire)

2 comments:

Maoni yako