October 17, 2012

MITI NI UHAI, KILIMO NI UHAI

Picha ya 1: mradi wa umwagiliaji maji katika kijiji cha Lundo. mradi huo umekamilika kadiri ya mkataba baina ya Wakulima na wawezeshaji. mradi huo umeanza kutumika ili kuwezesha zao la kilimo cha Mpunga kufanyika kwa urahisi. Mavuno ya zao hilo huwawezesha wakulima kupata faida kiuchumi na kujiongezea kipato. Mpunga ni zao linalotegemewa kwa kiwango kikubwa katika wilaya mpya ya Nyasa.

Picha ya 2 chini: miche ya miti katika kijiji cha Kitanda. Wilaya zote za mkoa wa Ruvuma zipo kwenye harakati za kuhakikisha mkoa huo unakuwa na mandhari mazuri na mazingira yanalindwa kwa kuhimiza upandaji miti.
Kilimo cha umwagiliaji kimeendelea kushika aksi katika vijiji mbalimbali katika wilaya ya Nyasa. hapa ni moja ya mifereji ya kupitishia maji ili yaingie shambani.
PICHA na Hoops Kamanga

No comments:

Post a Comment

Maoni yako