January 11, 2013

CCM IMERUHUSU YENYEWE KUKABWA KOO NA UPINZANI


Na Markus Mpangala, Dar es Salaam

Kuna dhana moja kwamba vyama vya upinzani ni uadui. Kimsingi jambo hilo sio kweli na lazima tukemee kuwa kazi ya vyama vya upinzani ni kuikumbusha serikali kupitia chama kinachotawala. Hivyo basi kazi ya serikali ya CCM ni kuhakikisha kuwa masuala ya msingi ndani ya nchi yanafanyika ipasavyo. 
Haiwezekani wapinzani wakaibuka tu kutoka porini na kuanza kupinga ama kulalamikia jambo fulani. Lazima wameketi chini na kuona namna ambavyo CCM inakosea na makosa hayo ni dosari tu ambayo inatakiwa kufanyiwa kazi. Vivyo hivyo kazi ya CCM sio kulalamika kuwa kwanini wapinzani hawashiriki kutatua kero ya nchi yetu. Kazi ya vyama vya upinzani ile kukosoa na kukishambulia CCM maana yake wanatimiza wajibu wa kuikumbusha serikali ya CCM kuwa kuna mahali hapaendi vizuri. 
Kwahiyo Kazi ya mpinzani ni kukupinga. Dosari yako ni faida kwake. Yapo maeneo ambayo vyama vyote vinapaswa kushirikiana, mathalani lile kongomano lililoandaliwa na ofisi ya msajili wa vyama vya siasa kuhusu ulinzi, usalama na demokrasia, mbali ya Chadema kususia. Lakini neno kubwa hapa ni kwamba mpinzani akiona dosari zako ndio kete yake ya kupata ushindi.  
Ukitaka mpinzani wako asipate kete ya ushindi hakika unaziba mianya yote ya kumfanya apate kete. kwanza, hakika Ilani ya chama chako inatekelezwa, ahadi zote zinatimizwa. njia mpya za uchumi zinavumbuliwa maana watalamu wapo. mkondo mpya wa kuibua maendeleo unatakiwa kupatikana, vivyo hivyo unapaswa kuelewa kuwa anayesababisha vyama vya upinzani kupata la kusema ni chama tawala chenyewe. 
CCM ikijikita kwenye shughuli za kutimiza maazimio yake kwa wananchi, sidhani kama ni vibaya. MTAJI KISIASA, inawezekana hata Mheshimiwa mbunge wa Nzega alipokemea kuhusu uchimbaji madini na kuhimiza watu kugoma ni MTAJI PIA. Sijui wanasiasa wetu wanatafsiri namna gani juu ya mtaji wa kisiasa. Na kugoma ilikuwa hatua ya mwisho pale Nzega mjini Tabora ili serikali isikilize kilio cha wachimbaji wadogo wa madini. MUHIMU; CCM timizeni mliyokusudia kwa maendeleo ya wananchi. do it all utaona kama akina sisi huku pembeni kama tutakosoa. Ni faida kwenu na kwa wananchi sisi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako