January 11, 2013

WILAYA YA MBINGA YAENDESHA KAMPENI YA UPANDAJI MITI

Ambroce Nkwera, Mbinga
Na Ambroce Nkwera, Mbinga

Wilaya ya Mbinga imeendendelea na kampeni kubwa ya upandaji miti kwenye maeneo mbalimbali ya wilaya hii. Hatua hii inalenga kulinda na kuhifadhi mazingira ya wilaya Mbinga ikiwemo kupambana na mabadiliko ya tabia nchi. Wananchi mbalimbali walijumuika katika kapeni hii ambayo imewahusisha watu wa kada mbalimbali, maofisa wa serikali na asasi binafsi wilayani hapa.
Wananchi wamehimizwa sana umuhimu wa kupanda miti kila wanapokata na hata pale wasipokata. kwa mujibu wa azimio la Halimashauri ya Wilaya Mbinga, kila mwananchi anataiwa kushiriki ikiwa sehemu ya mipango ya maendeleo ya uchumi kwa kulinda mazingira ya wilaya hii. mwandishi wa Habari hizi amefanikiwa kupata miti 700 ambayo amefanikisha kusafirisha hadi kijiji cha Mkali kilichopo katika wilaya ya Nyasa kwa lengo la kuendeleza kampeni ya kupanda miti. 
Kwa mujibu wa ratiba ya kampeni ya upandaji miti, itapita katika vijiji mbalimbali vinavyounda wilaya ya Mbinga huku uwezekano wa kampeni hizo kuhamia wilaya ya Nyasa ni mkubwa. Ikumbukwe kuwa wilaya ya Nyasa ni mpya ikwia bado inategemea watendaji kutoka wilaya ya Mbinga, hivyo kampeni hizo zitakwenda sambamba na uhamasishaji wa utunzaji mazingira kwa wilaya ya Nyasa ili kuepuka ukame unaoweza kutokea. Kampeni hii imevutia wengi na wananchi wamepanda miti ya kutosha.
Kulikuwa na mkakati wa upandaji miti na bado unaendelea, awamu ya kwanza waliotesha miti laki nne(400,000) yote wakawagawi wananchi bure na ikaisha awamu ya pili ndio hii, pia wamegawa miti karibu laki moja(100,000) na imeisha. Wananchi wameitikia mwito huu kwa ari kubwa sana. Tumegundua kuwa wananchi walikuwa wakikosa msukumo hivyo hatua hii imesaidia zaidi kufanikisha kusambaza habari za utunzaji wa mazingira kwa maendeleo yao.
Mipango mingine juu ya kusambaza na kuelimisha umuhimu wa upandaji miti inaendelea hapa Mbinga, huku halmashauri ya Wilaya kwa kushirikiana na baraza la Madiwani na wabunge wake kuhakikisha mpango huu unakwenda safi na kuboresha mazingira. Aidha, tunatarajia mpango huu utafikishwa hadi wilaya ya Nyasa kama ilivyokusudiwa ili kukabiliana na ukame, pamoja na kuhifadhi mazingira. Tunawakaribishana wana Mbinga wote kutimiza ajenda hii ya kutunza na kuendeleza mazingira ili yawe bora kwa afya bora. Hilo litasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako