January 12, 2013

WANAWAKE NA WANAUME: HAKI SAWA NA USOMI

Jackline Mluge, Finland

Na Jackline Mluge, Finland

WANAWAKE VIPI? katika ulingo wa ndondi kuna raundi 1 hadi 12. zamani wakati raundi moja kwenda nyingine inapokwisha, kuna wanaume walikuwa wamevishwa suti au mavazi safi kutangaza raundi inayokuja ni ya ngapi. 
SIKU hizi WANAWAKE wanatumika kutangaza raundi huku wakiwa wamevishwa vichupi, au mavazi ambayo yanaonyesha nusu uchi kabisa, wanatembea kwa mikogo sana. Nini hicho? 
Hapa bongo utaona WANAWAKE wanavaa visuluwali vya mazoezi na kugeza kuwa mtoko wa siku, wanasema fasheni. Kila sehemu ya mwili huonekana, kama minyama au kiuno maridadi na kadhalika. WANAWAKE mnajidhalilisha ama? naendelea ....
Sasa hivi wanawake wanafanya kazi zote ambazo wanaume wanafanya. Ilikuwa zamani lakini si kwa sasa ila wanaume ndio wanao ji dhalilisha kwa sasa unakuta dumezima lina baka mtoto.Mimi na pingana kabisa haki sawa kwa jinsia zote
simpenzi wa nguo fupi lakini nadhani kila mtu ana uhuru wa kuvaa anachotaka hiyo siyo kujidhalilisha. 
Na kuhusu kujiuza kuna wanaume wanajiuza kwa akina mama wenye pesa tena wanapanga mstari unachagua kama nguo, na sasa wanawake wanajibadilisha kuwa wanaume na wanaume wanajibadilisha kuwa wanawake. Hao wanafunzi wanaojiuza wamezoea kujiuza sisababu hawajapata mkopo- mfano nasoma chuo cha Afya napata hela kidogo kutoka serikalini lakini muda wangu wa ziada nafanya kazi ya fani ninayosomea au hata nyingine kujipatia hela za matumizi na wakati huohuo na soma. 
Naamini unapokuwa chuo si mtoto tena umefikia umri wa kujitegemea kiamawazo lakini nia aibu mtu mzima kufundishwa kuacha umalaya, Hebu niambie wakimaliza chuo wasipopata kazi watalalamika kazi hakuna ngoja tuendelee kujiuza. 
Limenisikitisha sana kuona watu wenye elimu bado wanakili za kulalamika kitu fulani badala ya kuchagua njia mbadala ya kutatua matatizo yao mfano mnaweza kuanzisha kuuza sambusa hostel unajipatia pesa tatizo la wasomi wa Tanzania mtu akifika chuo hataki kufanya kazi mbaya mbaya anataka kufanya kazi hiyo hiyo aliyosomea huku kuna watu wanasomea uanasheria au uganga nk lakini utakuta wanafanya kazi ya kuuza baa kipindi wanasoma wakijipatia hela za kujikimi na mtu aoni aibu.Tanzania ehiii amka sasa acheni porojo.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako