January 15, 2013

MIKOA YA MTWARA,LINDI NA RUVUMA TAFUTENI SULUHU KUFELI MITIHANI

Na Hamisi Magendela , Dar es Salaam
SIKU chache zilizopita wananchi wa mikoa ya kusini waliandamana kupinga uchimbaji wa bomba la gesi kutoka huko kwenda Dar es Salaam ambacho ingetumika kwa ajili ya kuzalisha umeme.
wanafunzi wakiwa darasani katika moja ya shule za msingi wilayani Nyasa
Umeme huo ambao ungezalishwa jijini Dar es Salaam ungetumika katika mikoa mbalimbali ya Tanzania hali ambayo inaaminika kuwa itasaidia kupungua ghalama za umeme na kufanya ukali wa maisha kupungua.
Sipingi mawazo yao kwani kila mmoja anafikilia kwa utashi wake japo ni vema wakaangalia faida kuliko na mafanikio yatakayopatika siku za usoni ikiwa gesi hiyo itasafilishwa kwa njia ya bomba kwenda Dar es Salaam.
Kikumbwa ambacho naweza kusema ni kwa wananchi wa mikoa ya kusini wanatatizo makubwa zaidi ya kuandamana kutaka manufaiko ya gesi wakati suala zima la elimu likiwa limewatupa mkono kiasi kwamba inatia simanzi kuona inashika nafasi 10 za mwisho katika ufauru wa matokeo ya kidato cha pili yalitangazwa juzi na Wizara ya Elimu na Mafunzo jijini Dar  es Salaam jana.
Licha ya kuwa ni aibu kwa wananchi pamoja na viongozi wa mkoa huo lakini naweza kusema kuwa ni kashfa ambayo katika miaka 50 ya Uhuru ijayo inatakiwa kufanyiwa kazi ili kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha na kuondoka na ujinga wa kukosa elimu.
Ingekuwa vema zaidi badala ya kulalamikia kuhusu gesi wangepiga kelele kwa kukosa elimu bora kwa wanachi wengi wa mikoa hiyo hali inawafanya kukosa nafasi nzuri katika viwanda vinavyojengwa katika mikoa.
Kwa maana nafasi nzuri ya ajira itakuwa ikishirikiliwa na wageni ambao wana elimu ya kutosha ya kukidhi mahitaji ya kazi inayohitajika kwa wakati huo na kufanya wenyeji kufanya kazi za hali ya chini kila siku.
Pia wananchi wa mikoa ya kusini umefikia wakati wa kusimama kidete kuhakikisha fursa iliyotangazwa na Serikali kuwa kuanzia sasa hakutakuwa na mwalimu atakaepangiwa kazi mijini kwa wanaotoka vyuoni.
Kwa maana hiyo ikiwa viongozi wa mikoa hiyo wakitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi wa kuzingatia elimu badala ya kung'ang'ani masuala ambayo kwa sasa hayasaidii sana katika miaka 50 ijayo.
Kusudio hilo la Serikali kupeleka walimu vijini linatokana na malalamiko kutoka sehemu hizo kuwa zimesahaurika kielimu kutokana na kukosa walimu wa kutosha hali inayofanya mikoa hiyo kushikia mikia katika matokeo ya mwisho kama ilivyo sasa kwa mikoa ya kusini.
Serikali kupitia Wizara ya Elimu ilisema lengo la kufanya hivyo ni kupata uwiano wa mwalimu mmoja kwa wanafunzi 10 hali itakayosaidia kunyanyua kiwango cha elimu katika mikoa iliyo pembezoni mwaka nchi.
Hivyo naamini fursa hiyo ikiwa itatumiwa vema na wananchi wa huko itafanya viwanda vinavyojengwa sasa katika mikoa hiyo wenyeji kunufaika kazi zaidi kuliko wageni ndio madhumuni makubwa ya baadhi ya wawekezaji.
Kwa maana wapo wanaotoa ahadi kuwa ikiwa viwanda vyao vitamalizika waajili wenyeji kwa asilimia zaidi ya 60, lakini ikiwa hali ya elimu itaendelea kuwa hivyo ni dhairi wageni watakuwa na nafasi kubwa kuliko wazawa.
Viongozi wa mikoa ya pembezoni mwa Tanzania ikiwemo ya kusini kazi kwenu kuhakikisha mnahamasisha wananchi wenu wanatumia fursa inayotolewa na Serikali kupeleka walimu vijijini inatumiwa vizuri na matunda yaonekana.
Pia kwa Serikali ni vema ikatambu kuwa si walimu pekee wanahitajika katika mikoa hiyo iliyo pembezoni mwa Tanzania bali vyenzo za kufundishi nazo ni muhimu, itakuwa haina maana kupeleka walimu bila ya vitendea kazi na kuwajengea miondo mbinu mingine ikiwemi malazi bora.
Kwani upo uhushuhuda kuwa walimu wengi wanakacha kwenda kufundisha vijini kutokana na kutopatiwa mahitaji muhimu ya kibinadamu ikiwemo usafiri, nyumba nzuri za kuishi na kuishi katika maboma.
 Maoni: 0782839898

No comments:

Post a Comment

Maoni yako