March 09, 2013

MATOKEO YA UCHAGUZI NCHINI KENYA: NI UHURU KENYATTA


Dorine Otinga
Na Dorine Otinga, Eldoret, Kenya

Matokeo ya uchaguzi yameshatangazwa huku Uhuru Kenyatta kutoka muungano wa vyama vya Jubilee akitawazwa kuwa rais mpya wa Kenya baada kumshinda Raila Odinga wa muungano wa CORD. Uhuru amepata 50.1% na Raila Odinga 44.3%.

Bila shaka tarehe 4 Machi ni siku ambayo itasalia katika kumbukumbu za wakenya. Ni siku ambayo Wakenya walijitokeza kupiga kura kwa wingi. Kulikuwa na foleni ndefu katika kila kituo, ambayo ni dhibitisho la kutosha kwamba walitaka yule watakae mchagua awe mshindi.

Tume ya IEBC nayo ilifanya mipango kabambe kuhakikisha kwamba inatoa matokeo ya kweli. Korti za Kenya zilifunguliwa masaa ishirini na nne ili kukabiliana na yeyote atakaye vunja sheria. Wasimamizi wote wa IEBC walilala katika vituo vya kupiga kura. Kuna karani mmoja kutoka maeneo ya Kitui ambaye alitiwa mbaroni kutokana na kupeana karatasi mbili za kupiga kura kwa mtu mmoja.

Wale walioenda kinyume na sheria walichukuliwa hatua kali. Shughuli hii ya kupiga kura ilifanywa kwa amani na hali ya usalama ilikuwa shwari. Kura hizi zìlihitajika kuhesabiwa katika kila kituo na matokeo yake kuwasilishwa kupitia njia ya kielektroniki. Shughuli hii ya kuhesabu kura ilikuwa imeanza kupitia njia ya kielektroniki,ambayo ilikuwa ya haraka lakini ikafutiliwa mbali na mkurugenzi wa tume ya IEBC, huku akidai ilikuwa na mushkil kidogo.
    
Ilibidi wasimamizi wa kila eneo bunge kupeleka matokeo ya eneo lao katika kituo kikuu cha kuhesabu kura cha Bomas of Kenya. Ilibidi maafisa wa tume huru ya IEBC kufanya kazi hii kupitia njia ya dijitali.Vyombo vya habari vilifanya kazi kubwa ya kuwasilisha matokeo yaliyokuwa tayari. Matokeo haya tangia mwanzo yalionyesha kuwa Uhuru Kenyatta alikuwa akiongoza  huku Raila Odinga akimfuata kwa karibu. 
          
Kulingana na takwimu za IEBC, Uhuru Kenyatta alipata kura nyingi kutoka maeneo ya Rift Valley na Central Kenya , miongoni mwa maeneo mengine. Raila Odinga naye alipata kura nyingi kutoka maeneo ya Nyanza, Western, na Pwani.Hii ni taashira kwamba  ukabila bado upo. Mgombea kiti mwingine Musalia Mudavadi alikubali kwamba ameshindwa na kuahidi kwamba yuko tayari kumpongeza yule atakayeshinda. Peter Keneth vile vile alisalimu amri.

Kulikuwa na tetesi kutoka upande wa Raila kuhusu jinsi kura hizi zilihesabiwa. Aliyekuwa Makamu wa Rais Kalönzo Musyoka alisema kuwa kuna sehemu ambazo zilisomwa ambapo idadi ya wapiga kura lilipita idadi ya waliojisajili. Jambo hili lilipingwa vikali na Bwana Isaac Hassan,mkurugenzi wa IEBC, ambaye alisema kuwa hajaona suala hilo, na iwapo kutakuwa, angefutilia matokeo hayo mbali.  
          
Uhuru Kenyatta
Hapo jana, kuna kundi kutoka utumishi wa umma, ambacho kiliwasilisha malalamishi yake Mahakamani, huku likitaka matokeo ya uchaguzi kufutiliwa mbali na waanze upya.

Waliweza kuambiwa wapeleke malalamishi yao katika mahakama ya juu kulingana na katiba. Kwa upande mwingine, mgombea mwenza Uhuru, ambaye ni Wiliam Ruto, alipongeza na kushukuru tume huru ya IEBC kwa kazi nzuri. Licha ya tetesi hizi zote Wakenya walionekana watulivu na kuwa tayari kumkaribisha Rais mpya. Walifurahishwa na uwazi ambao ulikuwa katika tume hii. 

Mnamo usiku wa tarehe nane, tume hii iliweza kudhibitisha kwamba Uhuru Kenyatta alitimiza asilimia hamsini ukiongeza moja, ya kura zote, jambo ambalo mgombea urais anafaa kutimiza ili kuwa Rais kulingana na katiba ya Kenya.  ingawa hakuwa amefikisha asilimia hamsini ya kura zote.

Uhuru Kenyatta alipata kura milioni sita nukta moja  huku Raila akipata kura milioni tano nukta tatu. Kura zote zilizopigwa ni milioni kumi na mbili nukta tatu. 

Tume ya IEBC, iliahidi kuwasilisha matokeo yake pindi tu watakapokuwa tayari kupitia mkurugenzi wao. Kwa upande wake,Uhuru Kenyatta aliandaa jukwa lake,katika Chuo Kikuu cha Kikatoliki cha Afrika Mashariki, mjini Nairobi huku akisubiri matokeo haya yasomwe rasmi, ndipo atoe hotuba yake.
Katika ukumbi huu,aliwaalika wagombea wengine walioshinda. Asubuhi ya kuamkia leo, imekuwa ni shangwe na hoi hoi kutoka kwa wafuasi wa Uhuru. Licha ya hayo, wakenya wameonywa kutokana na matamshi ya chuki na uchokozi miongoni mwao.

Kwa upande mwingine, Raila Odinga akitoa hotuba yake baada ya kutangazwa kushindwa uchaguzi dhidi ya Uhuru Kenyatta, alisema anakusudia kupeleka malalamishi kuhusu Tume ya IEBC na anasema ataenda supreme court. Pia alisema kuwa kuharibika kwa vyombo siku ya uchaguzi ilikuwa mpango na anasema ana imani na mahakama ya juu. Raila anasema  kuwa ajenti wake walitolewa nje wakati wa kuhesabu kura jambo ambalo ni kinyume na sheria.

Odinga, amesema kuwa atakubali uamuzi wa mahakama ya juu na kuwa ana ushahidi wa kutosha katika malalamiko yake. Lakini amewaomba wafuasi wake kutulia kwani hangependa ya 2007 kutokea tena.amemaliza kwa kusema kuwa haki itatendeka.

Dorine Otinga ni mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Egerton nchini kenya, akisomea Shahada ya Elimu katika lugha ya Kiswahili.

1 comment:

  1. Every weekend i used to pay a visit this web
    site, because i wish for enjoyment, since this this web page conations really
    nice funny data too.

    Here is my homepage ... gay4all.nl

    ReplyDelete

Maoni yako