December 10, 2013

JE MAPATO YA DAR PORI YANADHIBITIWAJE NA HALMASHAURI YA WILAYA YA NYASA?



Na Vitus Matembo, Mbamba Bay
 
Leo kilio changu kipo katika kijiji cha Dar Pori au jina jingine Runyeli. Ambako ni maarufu sana kwa machimbo ya madini. Hali ya maisha huko ni ya juu sana ukilinganisha na maeneo mengne wilayani Nyasa. 

Maisha yapo juu ila huduma muhimu hakuna HOSPITALI, Usafiri  na Kituo cha POLISI. Kijiji kipo kilomita 8 kuingia Msumbiji, sasa wakazi wa Dar Pori wanalindwaje?


 Wakiumwa hupelekwa Zahanati ya Mpepo iliyopo kilomita 20 toka kijiji cha Dar Pori. Kijiji hicho kina takribani watu 6000 wengi kuliko hata wakazi wa Mbamba Bay na Liuli, ila watoto wanaokwenda shule ya msingi ni wachache sana, kwa mfano waliofanya mtihani wa darasa la 7 mwaka huu ni 11 tu.
 
Sambamba na hayo yote,hebu tujiulize WANYASA wenzangu mapato yanayopatikana katka machimbo ya kijiji cha Dar Pori yakwenda wapi?,
Mpaka sasa hakuna geti lolote la ukaguzi wa bidhaa na malighafi zinazoingia na kutoka katika eneo hilo? Pia wakazi wa maeneo ya Tingi, Kingerikiti na Dar Pori kila kitu hutegemea kutoka Mbinga na si wilaya ya Nyasa, Je tutapata chochote ?
Halmashauri yetu itafute namna ya kukusanya mapato yatokanayo na machimbo yaliyopo kijiji cha Dar Pori.
"PAMOJA TUIJENGE NYASA"

1 comment:

  1. Asante kwa taarifa, ingawa inaumiza roho. Picha zinavutia.

    ReplyDelete

Maoni yako