June 27, 2014

MRADI WA KUFUGA KUKU WA KIENYEJI



Na Vitus Matembo, Mbamba Bay 

Wilaya Nyasa imeendelea kushuhudia mipango ya maendeleo baada ya asasi ya kiraia iitwayo Tanzania Agricultural & Livestock Promotion Association (TALIPA) kupewa kibali na serikali kuhudumia na kuhamasisha wananchi wa Nyasa juu ya ufugaji wa Kuku.

Taasisi hiyo inahamasisha Wanyasa kufuga kuku kwa wingi wakipatiwa matibabu na kuhudumiwa kwa miaka mitatu mfululizo. Inaonesha kwamba kwa kuku mmoja unaweza kupata sh.1,444,000/= kwa mwaka. Kuku hawatakufa kwa kideli wala tatizo lolote.

Hivyo gharama ya kujiunga ni sh.15,000/= kwa kila mfugaji ili kupewa Semina na Huduma bure ya kuku wako. Hivyo TALIPA inashirikiana na kaya katika kufuga Kuku wa Kienyeji.

Hilo limefanyiwa tafiti na kuonekana kwamba kwa kuku mmoja atataga mayai 10 na kutotoa kwa kila miezi miwili. 20% watakufa ambapo watabaki vifaranga 8, ambapo baada ya miezi 6 , kuku mizao miwili kwa jumla ya kuku 16 na mama kuku mmoja watataga mayai takribani 17*8. Hvyo gharama ya chini ya kuku mmoja ni sh. 7000/= ambapo mara hao kuku zaidi ya 200 utapata faida hiyo.

NB: Mazingira na usafi ni muhimu ili kupata kuku wengi zaidi.

TUNAOMBWA TUSHIRIKIANE NAO ILI KUONDOA UMASKINI KWETU NYASA.
Kwa mawasiliano piga simu na:0717554488

No comments:

Post a Comment

Maoni yako