September 27, 2017

HOJA 10 ZA WABUNGE WA CHAMA CHA NRM


KAMPALA, UGANDA

1. Acha "Mamlaka ya Raia" iamue. Kuweka ukomo wa umri ni kuwanyang'anya ni kuwanyima mamlaka yao ya Kikatiba.
2. Uhuru wa Raia kuchagua wampendae uheshimiwe. Kama hawampendi kura zitaamua.
3. Ibara inayoweka ukomo ukomo wa umri ni ya kinyume na inakiuka ibara ya 32 ya Katiba inayokataa unyanyapaa.
4. Katiba si msahafu, sio vibaya kufanyia mabadiliko ibara husika.
5. Mfumo wa vyama vingi unatoa nafasi kwa kila Chama kusimamisha mgombea wanayemtaka, ni kinyume Chama kingine kuwaingilia.
6. Uganda inapaswa kuiga Israel wanaoruhusu yeyote anayeonekana kulifaa Taifa hilo kugombea bila vikwazo.
7. Miaka 75 ni ajali, haina uhusiano na kupungua kwa uwezo wa kuongoza.
8. Uganda si kisiwa, Nchi nyingine Afrika hazina zuio hilo la kipuuzi.
9. Binadamu anastahiri burudani nzuri kutoka mtu mahili.
10. Uganda ni mdau muhimu katika mahusiano ya Kikanda, haiwezi kujinyima fursa ya kuongozwa na kiongozi mahili na anayejua siasa za Afrika.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako