October 21, 2017

TABASAMU NA KITABU


Ragin Mmbanga (kushoto) na Markus Mpangala (Kulia)
Huyu ni rafiki yangu. Anaitwa Ragin Mbaga, ila tuwapo farashani hupendelea kumwita "Mzee wa bustani ya usomaji". 


Kitu kimoja kwetu tunapenda kusoma vitabu. Tunapenda kuandika andika maarifa. Tunapenda kusambaza upendo kupitia usomaji wa vitabu. Tunajua jamii inaweza kupigana dhidi ya ujinga kwa kutumia silaha ya vitabu. Tunapenda kujifunza kwa waliotuzidi na hata tuliowazidi. Madhumuni yetu ni kuhamasisha usomaji wa vitabu kwa wote.  

Kitu kingine zaidi, tuna amani sana mioyoni. Mimi nasoma "Mbio za Jasusi" cha Frowin Kageuka na yeye anasoma "Ishinde tabia ya kughairisha mambo" cha Joel Nanauka. Katika maisha furahia na ukipende kile ufanyacho. Ni tiba maridhawa.

Markus Mpangala,
Morogoro,
Oktoba 10/2017.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako