October 23, 2017

URUSI, CHINA KUTAWALA BIASHARA DUNIANI



 
MOSCOW, URUSI

MIKAKATI ya serikali ya Urusi kuifanya China kama mshirika thabiti na muhimu kiuchumi umechochea kukuza sekta ya biashara na kufikisha asilimia 22 katika mapato yake.

Gazeti la The Moscow Times limesema kuwa ushirikiana wa karibu baina ya Urusi na China umechangia kuimarisha mapato katika biashara na kufikia kiasi cha dola bilioni 80 mwaka huu huku matarajio yakiwa ni kufikiwa dola bilioni 200. 


Taarifa zinasema kuwa ili kuongeza mapato zaidi China imepanga kuweka mfumo mpya wa sheria za fedha wenye lengo la kurahisisha mikataba ya kibiashara kati yake na Urusi pamoja na kuongeza umuhimu wa matumizi ya Yuan duniani. 

Takwimu zilizotolewa na serikali ya China Oktoba 13 mwaka huu zinaonyesha kuwa katika kipindi cha mwezi Januari hadi Septemba mwaka huu biashara kati yake na  Urusi imeongezeka kwa asilimia 22.4  ambayo ni kiasi cha fedha cha dola za kimarekani bilioni 61.4. Katika kipindi hicho hicho, usafirishaji wa bidhaa za Chinja kwenda Urusi umeongezeka kwa asilimia 17 ambacho ni kiasi cha fedha cha dola za kimarekani bilioni 31.4, wakati bidhaa za kutoka Urusi kwenda China zimeongezeka kwa asilimia 28.5 ambayo ni kiasi cha fedha cha dola za kimarekani bilioni 30 katika kipindi hicho hicho.

Aidha, imeelezwa kuwa katika kipindi cha mwezi Septemba biashara kati ya nchi hizo mbili zilifikisha dola za kimarekani bilioni 7.6, ambapo thamani ya bidhaa za China zilizopelekwa Urusi ni dola za kimarekani bilioni 3.79, wakati bidhaa za Urusi zilizopelekwa nchini China zimefikisha thamani ya dola za kimarekani bilioni 3.81.

Kiwango cha ushirikiano wa kibiashara kati ya China Urusi kwa mwaka 2016 kilipanda kutoka asilimia 2.2 sawa na dola za kimarekani bilioni 69.5. nchi hizo zimetajwa pia kuwa washirika wazuri wa masuala ya kijeshi na diplomasia.

Biashara kati ya China na Urusi ilifikisha kiasi cha dola za kimarekani bilioni 5 na bilioni 8 miaka 1990, lakini kumekuwa na ongezeko kuanzia wakati huo.
Malengo ya awali ya nchi hizo mbili yalikuwa ni kufikisha kiasi cha dola za kimarekani bilioni 100 kabla ya kukumbwa na mdororo wa uchumi mwaka 2008.
Takwimu hizo zinaonyesha kuwa malengo ya Urusi yapo mbali sana ukilinganisha nay ale ya Umoja wa Ulaya ambako biashara imekuwa ikiyumba miongoni mwa wanachama. Wakati ushirikiano wa kibiashara kati ya Urusi na China ukizidi kuimarika, hali imekuwa mbaya kwa nchi zilizopo kwenye Umoja wa Ulaya (EU).Biashara kati ya Urusi na Umoja wa Ulaya imeshuka kutoka Euro bilioni 330 mwaka 2014 hadi Euro bilioni 228 kwa mwaka 2016, huku wataalamu wa uchumi watabiri kuporomoka zaidi. 

Hilo lina maana kukua kwa biashara kati ya Urusi na China kumesababisha kuporomoka kwa biashara ya EU na Urusi. China inatarajiwa kuchukua nafasi ya EU kuwa mshirika muhimu wa kibiashara kati yake na Urusi ifikapo mwaka 2020.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako