November 10, 2017

SOKA LA WACHINA, LIKABORESHWA UINGEREZA

NA.HONORIUS MPANGALA

INASADIKIKA Polisi wa China walikuwa wanacheza mchezo uliitwa 'Tsh-u' ikiwa na maana ya piga mpira. Mchezo huo ulipenyeza Japan na maeneo mengine ya Roma. 

Soka lilingia Uingereza mwaka 1066 wakati wa utawala wa Mfalme William. Kutokana na wachezajj wengi kupata matatizo ya vifo mfalme Edward na wengine kama Richard walipiga marufuku na kutoka kauli ambayo Kwa yoyote atakayehusika au kuonekana anacheza soka atenda jela.


Mwaka 1848 ulifanyika mkutano katika chuo cha Cambridge na kutengeneza sheria 17 na kutumia maeneo yote ya Uingereza.Moja ya sheria ilikuwa kuruaha mpira ulirushwa Kwa mkono mmoja yaani 'throw- in'.

Klabu ya Sheffield Fc ndiyo ya kwanza kuanzishwa. Ilianzishwa mwaka 1855 ikiwa na katiba na sheria za Cambridge. Mchezo wa kwanza kuchezwa ilikuwa kati ya Sheffield fc dhidi ya wapinzani wao na watazamaji walikuwa ni 600.

Charles Aldo ndiye alikuja kuufanya mchezo wa soka kuwa wa kusimimua pale alipoanzisha mashindano Kwa vulabu mwaka 1871. Na klabu ya wanderers ikachukua ubingwa huo huku mchezo ukihudhuriwa na watazamaji 2000 waliolipa kiingilio cha paundi moja Kwa kila mtazamaji.


Ni Charles Aldo aliyefanya mpango wa kuandaa pambano la kwanza la kimataifa mwaka 1877. Ilikuwa kati ya Scotland dhidi ya England na matokeo ya mechi hiyo kuwa sare tasa(0-0) Ndio maana hadi sasa mechi za Scotland na England huwa ma msisimko baina yao Kwa kiasi kikubwa sana.

Mwaka huo wa 1877 ndio sheria ya kutumia dakika 90 ilianza kutumika.Pia katika goli uliwekwa mtambaa panya 'crossbar' badala ya kamba. Pia waamuzi wanaochezesha mechi kutokutoka katika timu zinazocheza yaani uwepo wa mahusiano kati ya mwamuzi na timu inayocheza.

Katika maamuzi awali sheria zilikuwa katika vitabu hivyo walicheza na pale ilipoonekana ni kosa mechi ilisimama na walikimbilia kufunua kitabu na kutazama sheria inasemaje na kufanya maamuzi.Na waliita Reference book na baadae ndo sheria zote ziliamuliwa na maamuzi Kwa kumwita referee wakilitohoa toka kwenye reference.

Klabu ya Preston Ndiyo ya kwanza kunyakua ubingwa wa ligi ya Uingereza mwaka 1888 ilipoanzishwa.Na sheria ya uwapo wa wachezaji wa kulipwa ilianzishwa. Misri ndio nchi ya kwanza kushiriki kombe la dunia kutoka bara la Afrika. Ilishiriki Kwa Mara ya kwanza 1934.

Yawezekana uliyajua ila nilikuwa nayakumbusha tu. Sasa nakuacha na maswali la kiuamuzi.Kama wewe ni mwamuzi wa soka wakati unachezesha mpira, mchezaji akamrudishia mpira golikipa wake na akaudaka ndani ya eneo la golikipa dhahiri atakauwa golikipa atakuwa amefanya kosa. Je ni adhabu gani utakayoitoa?

Je unajua kwanini magolikipa wengi baada ya kuudaka mpira huwa wanapenda kuudundisha unajua maana yake kwanini wanadundisha mpira?

0628994409

No comments:

Post a Comment

Maoni yako