November 10, 2017

MAJINA YA MITAA HUFANANA

Mtaa wa Muhoro

Pichani ni mtaa mmojawapo ulipo jijini Dar es salaam. Ni mtaa wa Muhoro. Katika kumbukumbu zangu mtaa kama huu wenye jina hili upo katika Kijiji cha Lundu, kilichopo Kata ya Mbaya, Tarafa ya Ruhuhu, wilaya ya Nyasa mkoani Ruvuma. Lundu ni miongoni mwa vijiji vyenye historia kubwa na kipo mwambao wa ziwa Nyasa. 

Kumbukumbu hizo za kihistoria zinaonyesha uhusiano wa watu na namna wanavyoingilia au kuathiriwa na maisha ya eneo moja kwenda jingine.
Hakuna taarifa rasmi inayosema mtaa wa Muhoro wa Dar es salaam ulianzishwa kwasababu gani, sambamba na ule wa kijiji cha Lundu.  

MUHIMU: Kuanzia mwaka huu tutakuwa na habari kemukemu za kihistoria kuhusiana na ukoloni,wamisionari,wangoni na mengineyo katika mwambao wa Ziwa Nyasa (husuani Tarafa ya Ruhusu).
Endelea kubaki nasi…
Honorius Mpangala akiwa na Alfred Mpangala katika kibao chenye jina la Mtaa wa Muhoro jijini Dar es salaam

No comments:

Post a Comment

Maoni yako