November 15, 2017

ULINZI WA FAMILIA UPO MIKONONI MWETU

KATIKA kitabu hiki….. mhusika Ttiisa anafungua albamu. Ina picha nzuri kila anapofunua. Moja kwa moja anatupia jicho picha ya Suuna.Ni Suuna kipenzi chake. Aliyeingia nae penzini kwa miaka miwili (sasa), bila kujali namna Suuna alivyoleta ugonjwa wa Ukimwi ktk penzi lao (mechi za ugenini?).
 
Katika albamu hiyo hiyo Ttiisa anatazama pia picha ya Ggenza, mtoto wake aliyekuwa na umri wa miezi minne tu lakini alifariki dunia. Kulikoni? Riwaya inakupa jawabu
**************
Ttiisa ana ukimwi. Amekutana na Dona ambaye hana kazi (hana ajira wala hajajiajiri). Makutano yao yanaleta matatizo makubwa ambayo ni somo kwa maisha ya Kampala ya leo (Uganda). Maisha yao hayaeleweki. Sasa walifanyaje hadi kueleweka? ...
Ndo utamu wa nakala ngumu(hard copy) unafunua ukurasa mmoja hadi mwingine kisha unapambia mate kwa mbaaaaali....
#ThanksMolio.B.#

No comments:

Post a Comment

Maoni yako