January 11, 2018

KUFUNGWA KWA BENKI TANZANIA.

NA LAMECK KUMBUKA, USWISI
BENKI zinafungwa sio ishara njema kwa ucuhumi, lakini tufikirie pia sababu nyingine mbali na lile tunaloshabikia sana la “kuporomoka kwa uchumi”. Unajua kuwa idadi ya watu wenye simu na idadi ya watu wanaotumia huduma ya pesa kwa simu imepita zaidi sana idadi ya watu walio na Account benki?
Benki nyingi zilikuwa zinategemea wateja wa kawaida, amabao ndio idad kubwa ya watanzania. Bahati mbaya  Benki nyingi zilishindwa kujibu matakwa ya watu wa kijijini ambao ndo hufanya idadi kubwa ya watanzania wengi (hata wale wanaoishi mjini, wako Connected sana na ndugu jamaa marafiki, na miradi yao vijijin. Kile kilichoshindwa kufanywa na benki hizo, kinafanywa na huduma za simu, Mzunguko wa pesa umehamia kwenye simu sio tena katika mabenki.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako