January 12, 2018

SERIKALI YA BOTSWANA YAMKOROMEA RAIS TRUMP


NA MWANDISHI WETU

SERIKALI ya Botswana kupitia Wizara ya Mambo ya Nje imetoa taarifa ya kulaani matamshi ya rais Donald Trump dhidi ya wahamiaji kutoka bara la Afrika.
 
Kwa mujibu wa taarifa ya wizara hiyo iliyotumwa kwa vyombo vya habari ilisema, serikali imeamua kumwita balozi wa Marekani nchini humo ili kutoa ufafanuzi juu ya matamshi ya Trump na kueleza nafasi ya Botswana katika kundi lililomaanishwa na rais huyo wa Marekani.


“Leo (jana) Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa imemuita balozi wa Marekani hapa nchini kutoa ufafanuzi dhidi ya matamshi ya Rais Trump kuwa nchi za Afrika na nyingine ni kama uchafu, katika kikao cha Kamati ya Wabunge wanaoshughulikia masuala ya uhamiaji,

“Serikali ya Botswana pia imetaka ufafanuzi kutoka serikali ya Marekani kupitia Balozi huyo na kuthibitisha kama nchi yetu ni miongoni mwa uchafu unaotajwa,
“Botswana inaziomba nchi wanachama wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC), Umoja wa Afrika na nchi zinazoendelea kote duniani kulaani matamshi ya rais Trump,”

No comments:

Post a Comment

Maoni yako