February 19, 2018

HATUNA UWEZO HATA WA KUJENGA VYOO KWENYE ZAHANATI ZETU?

Zanahati ya kijiji cha Mbangamawe Kata ya Gumbiro wilyani Songea, imeshindwa kufanya kazi kwa zaidi ya miaka miwili tangu ilipojengwa kutokana na kukosa huduma ya choo. Hali hiyo inawalazimu wakazi 1350 wa kijiji hicho kukosa huduma za afya tangu kuanzishwa kwa kijiji hicho, hivyo wanalazimika kufuata huduma katika kijiji cha Ngadinda umbali wa kilomita 12.

Kufuatia tatizo hilo, Mkuu wa Wilaya ya Songea, Pololet Mgema, alifika katika kijiji hicho na kutoa mifuko 30 ya saruji kwaajili ya ujenzi wa choo, ili kutoa nafasi kwa wakazi hao wapate huduma za matibabu.

©Nipashe, Feb.19/2017.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako