February 07, 2018

WANAOACHANA KIDEMOKRASIA HUWA HAWAFUTI UPENDO NA MAPENZI YAO

NA HONORIUS MPANGALA
MAHUSIANO kuna nyakati yanashindwa kukupa tafsiri iliyo sahihi na ikakuumiza kichwa kwanini yanatokea unayoyaona. Yawezekana ulikuwa hujui na ukaona wewe ni mshindi katika haya matukio kumbe unajidanganya.

Kuna watu katika mahusiano huachana kwasababu ya kimazingira,mawasiliano,imani na hata kipato. Hawa Mimi nawaweka katika kundi la kuachana kidemokrasia. Kwani mioyo yao inakuwa bado kwa watu watu wao waliowapenda na huko kwingine waliko ni kutokana na hizo sababu nilizozisema.
Nianze na Mazingira, katika Maisha ya kawaida hutoe walioko katika mahusiano huweza kutenganishwa na mazingira na ikawa moja kwa moja wakaachana. Inatokea mmoja labda ameenda nje ya nchi au hata nje ya mkoa. Kitendo cha kuwa mbali na mwenzake kitamfanya aweze kuwa na Wa mazingira aliyopo kwasababu tu mahusiano yapo popote duniani.


Lakini katika hilo huenda ikawa kufanya vile ni kujaribu kwenda sawa na mwenendo wa Maisha kwa mazingira hayo licha ya kwamba uhalisia Wa mapenzi ukawa hauko sana eneo hilo.Inatokea Mtu anaoa au kuolewa katika mazingira haya. Kitu pekee cha kuamini ni kwamba kaolewa kwasababu ya mazingira hayo kwasababu kama ni matibabu ya kihisia yana mtu wake ambaye yeye ndo kila kitu kwake. 

Ikitokea siku akakutana na mtu wake ambaye aliachana nae kimazingira mfano katika maeneo ambayo mwenzake wake hayupo hakika nakuambia iwe ameoa au ameolewa,jambo la kwanza itakuwa kurejeshea hisia pale walipoishia kabla ya kupoteana kimazingira. 


Kitakacho fuata hapo ni kuweka ahadi ya kukutana au ikiwezekana muda huo huo mnara wa hisia unakuwa unasoma 4G na unakuta watu wanasimamisha shughuli na kutibu hisia zao ambazo wanajuana kuwa tangu awali hapa ndo ilikuwa mahala sahihi kwake. Tairi la treni halichengi reli.

Jambo la kimawasiliano hutokea katika hali ambayo inafanana na. Mazingira. Kwani yawezekana katika mahusiano mmoja ya wapenzi au wachumba akatoka eneo moja na kuwa eneo lingine. Sasa kufa kwa mawasiliano kinaweza kusababisha mahusiano kuvunjika. Lakini kuvunjika huko kunaweza kusababishwa na mawasiliano licha ya kwamba hao watu wanapendana sana. Baada ya kimya cha muda mrefu hutokea kila mmoja kubadili maamuzi kutoka hali ya kuzifuata hisia zake kama ilivyo kuwa awali na kufuata matibabu ya kibiolojia kwa kumpata mtu ambaye atakuwa na mahusiano ambayo wanafikia kuoana.

Sasa siku ikatokea hao watu walaiochana kwasababu ya kukosa mawasiliano ,hawakugombana wakaja kukutana katika mazingira ambayo hayakutarajiwa ujue mshtuko mkubwa utatokea baina yao. Mshtuko huo hauwezi kuzuilika hata kama hawa watu watakuwa na wenza wao. Kitakacho sababisha mshtuko ni mwili kurejea katika hisia za kweli juu yao huku akili ikirejea nyuma haraka na kukumbuka yaliyokuwa yanafanyika katika mahusiano yao. 

Hapo hata iweje kila mmoja atakuwa na lawama juu ya mwenzake. Huku wakiambizana nimeoa au nimeolewa. Lakini akili nyingine itawatuma kurejesha kile wakichokuwa wakikifanya kabla ya kuoa au kuolewa baina yao. Hapo lazima hisia za kweli zijenge hoja toka mwili wa mmoja kwenda kwa mwingine. Hapo ndipo utakapojua kuwa watu wameoa wake wasio wanawake zao,na wanawake waneolewa na waume wasio wanaume zao.

Hisia na mapenzi ya kweli hayawezi kuifanya dini ikashinda katika mahitaji ya watu wenye mahusiano ya kweli. Kinachofanyika ni kuilazimisha akili ikubali kuwa dini imepelekea mahusiano kuvunjika na hawa watu kila mmoja akachukua njia yake kuanzisha mahusiano mengine. 

Hapo tunajidanganya kwasababu hisia hazijawahi kushindwa mbele ya kile ambacho moja kwa moja kipo katika mwili au mtazamo wa mhusika. Itatokea mwanaume ataweza kuoa mwanamke kutokana na inani ya dini yake huku yule wa hisia zake akamua kukubali kuachanae hapo imetumika demokrasia ambayo imesababishwa na imani. 

Hata kwa mwanamke pia kutokana na msukumo wa watu wa karibu ataikubalia akili yake kuwa ataolewa na mtu mwingine tofauti na yule wa hisia zake ambaye aliziteka na kumfanya awe mfuasi kamili wa mahusiano. Lakini dini inaingilia na kutenganisha hili. 

Huyo mtu atakayeo oa au kuolewa naye itakuja siku ataonekans kama ni kituko kwa mwenzake. Hali hiyo itafanya nafasi ikipatikana hawa wapenzi wenye hisia za kweli katika mahusiano yao wakakutana iwe Stand ya bus,bandarini,sokoni hakika nakuambia lazima fikra za 'kuboost' zitawajia tu. Hii ni kutokana na kuachana kwao ni kwa kidemokrasia hivyo hawana ugomvi wowote hivyo kuifanya paredi ichangamke ni jambo la kawaida kwao. 

Hakika watatibu hisia zao kwasababu ya akili yao imereje katika wakati ambao matibabu yake yalikuwa muruwa na hakukuwa na msongo wowote utokanao na uhalisia wa mapenzi yao.Wataendelea kuibana kwasababu ya hisia zao zimepelekwa kwa watu ambao ni imani tu imesababisha.

Kipato nacho ndo jambo kubwa sana ambalo limetamalaki katika Maisha ya sasa.Watu hujaribu juzilazimisha hisia ziende sehemu ambayo ina kipato lakini kumbe uhalisia hauko hivyo. Kwani hisia hazitambui kipato zenyewe zinatazama namna ambayo huweza kumalizwa vyema na kumfanya mtu awe mwenye afya kiakili na kimaamuzi. 

Iko wazi utatuzi wa mambo atakao ufanya mtu aliyetoka kufanya mapenzi muda sio mrefu na ule wa yule ambaye hajafanya kwa kipindi utatofautiana. Inasemekana aliyetoka kufanya mapenzi anakuwa na utulivu mkubwa sana wa kiakili kwa wakati huo. Sababu kubwa ni kutokana na hisia kupata chakula cha kweli. Hii sawa na kitendo cha 'reboot' au 'back up' simu yako. Hivyo mtu akishafanya tendo hilo anakuwa kama ame reboot mwili na kuufanya unakuwa mwepesi wa kila kitu akili na mwili pia.

Sasa watu walioshindwa kufikia malengo yao sababu tu kipato ambacho kimesababishwa na pengine wazazi au wao wenyewe. Hakika kama watakuwa waliachana kidemokrasia basi hisia huwa hazijifichi. Ni Mara nyingi tunaona wanaume wakubwa wenye kazi nzuri mke ana kazi nzuri lakini huenda akawa na mwanamke mwingine ambaye hana chochote kile na wakawaida kabisa. Hizo hisia tena unaweza kukuta mwanamke Huyo alipikuliwa na mke wa Huyo mwanaume hivyo katika kuheshimu hisia unakuta bado wanakuwa na mahusiano. 

Wako wanawake ambai licha ya kuolewa na wanaume wenye kipato lakini bado wale ambao ndo hisia zao ziliko wataendelea kuwaweka katika kumbukumbu za akili zao. Mara waonanapo basi mzuka na hisia vinatanguzana pamoja. Hii inatokana na kushindwa kuzuia hisia zao ambazo zilijengeka tangu awali katika mahusiano yao.

Ukitaka kujua Watu wameoa au kuolewa na wanaume au wanawake wasio wake au Waume zao ni katika hili. Mara nyingi inapotokea mwanamke akiomba ruhusa ya kwenda kusalimia wazazi nyumbani kwao Onyo la mwanaume kwa mkewe ni "sasa ndo ukakutane na tuwanaume twako twa zamani eee" hapo utajua Kumbe akilini anajua kuwa wako wanaume wa zamani ambao waliteka hisia za mkewa kabla yake.

Ikitokea mwanaume ndiye anayeenda kusalimia nyumbani kwao utasikia mwanamke anasema " sasa huko ndo ukaonane na tuwanamke twako twazamani,nakuambia tutagombana". Kumbe akilini hili lipo na wanatambua kuwa wapo ambao waliifanya akili ya mume au mke kujisikia amani na faraja kabla tangu. Ndio maana makalipio kama haya yanatokea ili kulinda hisia zisiweze kuishinda akili. 

Wanaochana kidemokrasia suala la 'reboot' huenda lisiepukike kwasababu asilimia ya mahusiano yanayokufa moja kwa moja kuanzia akili hadi hisia ni Yale yalisababishwa na ugomvi baina ya pande mbili.

©Honorius Mpangala

No comments:

Post a Comment

Maoni yako