August 16, 2007

Blogu ni nini?

Nimeona ni vyema nikaweka hapa maana ya Blogu ili kuwezesha wengine wajifunze kama mimi nilivyojifunza.

Haya twende sambamba ili tusamabze maarifa kwa wengine.............
"BLOGU" ni neno la lugha ya kikoloni(kiingereza) limetokana na neno "Weblog".

"BLOGU" ni teknolojia mpya inayowezesha mtu yoyote,kikundi chochote au shirika lolote kuwa na ukurasa wake katika mtandao.

Hii ni kama shajara "notibuku" ya mtandaoni kazi yake ni sawa na ya vyombo vya habari mfano Magazeti,Redio,Runinga n.k.Aidha Blogu haihitaji kuwa na gharama zozote maana huduma hii ni bure.Bali kinachohitajika ni muda wako tu kuanzisha Blogu yako tena inakufanya utumie dakika 5 tu ili kukamilisha ndoto zako za kuwa na safu yako.

Hii inakuwezesha kuwa na safu yako mwenyewe kama vile ilivyo kwa wanasafu wa magazetini.Pia inahitaji wewe kuwa na hamu ya mabadiliko ya habari duniani,ambayo huenda mbio mithili ya upepo mkali lakini huu si upepo wa kupita bali ni upepo endelevu........maana hii nimeazima na imetolewa na kufundishwa mara kwa mara na......"Ndesanjo Macha" ;muone katika.."www.jikomboe.com'

Namna ya kuanzisha BLOGU yako.
Ingia hapa; HYPERLINK "http// mwongozo.wordpress.com,http//mwongozo.wordpress.com.

Blogu za kitanzania;ingia hapa; http//tinyurl.com/rwyow

No comments:

Post a Comment

Maoni yako