August 17, 2007

Unayajua maneno haya..

Inawezakana kwamba katika lugha yetu maridadi ikawa inachezewa na watu wasioelewa umuhimu wake.Wengi wanadhani kuongea lugha za Wakoloni ni njia salama zaidi ili kujiunga katikadunia tambarare hii..
Hebu tutazame maneno haya....

KISAGALIMA(vi-)=Ni jembe lililochakaa,kiselemo.

KIPWEPWE=Ugonjwa wa ngozi wenye kutoa madoa mekundu.

KIPETE=Kibahasha

MZAFAFA=Mwendo wa maringo.

NSONO-Tendo la kukoroma.

MNUMAMNUMA=Mtu apendaye sana kutafuta mambo ya uramali,mtukutu,apendaye kuulizia mambo ya uchawi,mshirikina.

MLEO (mi-)=Mwendo wa kupepesuka.

MGALABA(mi-)=Mshindani.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako