September 01, 2007

Uwongo si Mzuri..

Kuna jamaa hapa kanichezea sana,yaani nilijikuta natamani kumeza samaki mbichi kabisaa,unajua ni samaki gani 'mbasa'.Usishangae kwani huwezi kula samaki mbichi mpaka achomwe au kupikwa?

Jamaa kaniahidi kuniletea kitabu fulani hapa lakini matokeo yake hajaonrkana kwa kinyume na muda tulioahidiana wa saa 4,yaani nimengojea hadi saa 5 kasoro hivi jamaa haonekani.Aaaa nikaona huu sasa ni ujuha ngoja niongee na watu hapa kidogo lakini sina hasira naye kabisaa moyo uko safiiii....lakini si vizuri kudanganya kama masikini wa siasa na dhiki za siasa au vipi
u kwa vile mimi napenda sana vitabu na anajua kwamba nachukia sana uwongo...ananifanyia kusudi.

Aaa ndio huyu sasa anakuja huku mimi naandika waraka huu,eti anasoma..jamani ananikaripia,kwani mikono yake.....haya leta kitabu we' mbuni mnyasa feki maana jamaa anajiita mnyasa kumbe ....

1 comment:

  1. ndiyo kwani uwongo ni dhahabu,lakini tusowe kama wanasiasa...ni soga tu za hapa na pale

    ReplyDelete

Maoni yako