October 07, 2007

Ng'ombo;nyasa na habari zake

NG'OMBO ni kijiji kilichopo kandokando mwa ziwa nyasa.Kijiji huku kunapakana sana na Mtupale na kwa wasiofahamu wanadhani ni mtaa tu fulani huku wakijua mtupale ni kijiji kamili,kumbe hiki ni kijiji kamili na kina historia yake tokana wamisionari kujenga hospitali hapo toka zama zao za ukoloni na hadi leo inawasaidia wakazi wake.Shughuli kubwa hapa ni kama vijiji vingine yaani kilimo,uvuvi na ufugaji.Ni eneo lenye kupendwa sana na walevi kwani hujukusanya katika eneo lao la 'malini' kwa kujiburudisha au kushuhudia burudani mbalimbali za ngoma kama kioda,mganda,makanya n.k hizi ni ngoma za utamaduni ambazo huipendwa na wakazi wake.Uzuri wake ni kama vingine kwani hakuna uchafuzi wa hali ya hewa kama maeneo ya mijini,ni eneo linalofaa kwa kilimo cha mpunga ambacho wakazi wake wamekuwa wakijipatia kipato tokana na kilimo hicho.Ulimaji mwingine ni ule ulezi,mihogo na matunda.matunda ni mengi sana katika vijiji vya mwambao mwa ziwa nyasa tokana hali yake ya hewa kuruhusu ya baridi ambayo ni nzuri kwa kilimo chamatunda.Samaki ni wengi sana na dhana zitumikazo ni za asili mfano mitumbwi ambayo ni tegemeo kuu kwani huwezesha utunzaji na ulinzi kwa samaki ziwani.kifupi hiyo tu karibuni nyasa

No comments:

Post a Comment

Maoni yako