February 06, 2008

Fumbo katika Maisha kutoka Nyasa...

Jua limekuwa likitoka na kutua kila siku ya wiki iliyokwisha na litafanya hivyo hivyo katika wiki inayofuata.Mambo yataendelea hivyo bila kujali jinsi ninavyofanya au hata jinsi ninavyokuwa,Muda unapita na sote tunaona,wavivu kwa wachapakazi,wasiojali kwa wenye nidhamu hali kadhalika.Tunasimama katika mwanzo wa wiki hii,muda ambapo wiki mbili zinapokutana zinaweza kuleta harufu ya uchungu kwa baadhi yetu.
Uchungu wa kumbukumbu ya kushindwa kwa nyakati zilizopita,lakini pia inakuja na alama ya furaha kwetu sote kwa vile ni muda wa tumaini jipya linalofungulia mlango wa mafanikio mapya...Huu ni muda wa mafaniko mapya.
HEBU SASA TAFAKARI....Wiki iliyopita imepita,Hivi ilikuwa na maana gani kwangu?Inapokuja ilinikutaje?Na sasa imeniachaje?Na hapa inaanza wiki mpya nyingine.Je italeta nini au itaniletea nini?Hivi nitajisikiaje kadiri saa zake zitakapokuwa zinapita siku?Hayo yote ni fumbo kwangu kwa sasa....Hivi kila siku itakuwa na rangi gani?Na itaweka sura gani mbele yangu,kadiri nikitazama mshale wa saa ukisonga,hilo ni fumbo kwangu.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako