February 05, 2008

JANETI katua Nyasa na salamu yake "inyahi"....

Moja ya chanagamoto zinazowakabili ndugu zangu Wanyasa waliopo mijini na ughaibuni ni kuwaelimsha watoto wao mahali walipozaliwa wazazi.Chanagamoto hii ni kwamba wazazi wasije wakadhani kuishi mjini pekee ndiyo kunamfanya mtoto kujisikia vizuri zaidi ama kuwa na maarifa zaidi.Lakini mahala panapoitwa mjini ni mkusanyiko wa tamaduni mbalimbali ambazo Mwanafalsafa Karl Marx aliziita "Union Tribe" yaani muungano wa makabila kama ilivyokuwa huko Roma.Wazazi wetu hawa wanapaswa kuwaeleza watoto wao kwamba ni mahala gani walipozaliwa ili nao waweze kujionea asili ya wazazi wao ukizingatia hatari ya historia kupotea juu ya mambo kadhaa yatuhusuyo.Naam basi kama unavyojua wazazi wengine walivyo makini kuwafundisha watoto wao asili zao na utamaduni wake mfano angalia wachezaji kadhaa wa dunia hii waliozaliwa ughaibuni wanavyogeuka na kutafuta asili zao mfano Mwanasoka mahiri Frederic Kanoute wa Mali licha kuchezea timu ya Taifa ya Ufaransa aliamua kurejea asili yake.Hivyo kama kawaida Wanyasa kujivunia unyasa wao,mwezi januari katua dada JANETI hapa nyasa kwetu ikawa balaa yaani vumbi tupu,binti kachangamka licha ya kuona sisi Wanyasa kama 'katuni'{natania tu},jambo lake la kwanza ni kujifunza kusalimia kwa lugha ya Nyasa ukizingatia eneo alilokuwepo la MBAHA ni Wampoto kama ilivyo kwa LUNDU na maeneo ya karibu.
Wacha kabisa ndugu yangu huyu kaanza kuongea maneno kadhaa ya lugha ya hapa kasheshe tupu.Bahati mbaya neno lake lilikuwa moja tu "INYAHI",ingawa neno hili linamaanisha "nzuri" katika salamu ya neno "MONILE" lakini haliwezi kukaa katika kiitikio cha kila salamu,......acha kabisa dada katua kwa wanyasa yeye ni "INYAHI" tu wala haoni noma ndiyo kujifunza asili ya mzazi wake huko ni fahari sana katika afrika yetu.Kila salamu yeye ni "INYAHI" tu hakuna kikwazo yaani saaafi sana...Nyasa jamani yaani furaha sana najua akisoma hapa atanisaka tena hadi huku nyasa tunakovua samaki na kuzitafuna kiasili.....lakini nakupenda dadangu wala sikudhihaki ni kujielimisha huko.....natumaini atajifunza neno lingine mie sijui...acha ningoje nistabiri..

No comments:

Post a Comment

Maoni yako