June 02, 2008

Funzo La Mnyasa Hata Kama Humpendi

Wanyasa ni watu ninao waheshimu daima kwani wana msimamo juu ya maisha yao.Unaweza kumwona mnyasa akiwa kazini kama hivi ukadhani mshamba au mtu asiye na staha kabisa.Basi unajidanganya yaani utakuwa unacheka huku unalia wala usidhani kama natania.Hawa ni watu wanaopenda kufanya yale wanayoamini yanamanufaa kwa maisha yao,hawana haja ya kuharakisha maisha kwani wanajua kila kitu hupangwa na mungu huku ukiwa na uthabiti wa mipango hiyo.Sasa hebu angalia mwenyewe hapo nyavu ndiyo hiyo,matarajio ni kukomba mchuzi wa samaki wa aina yeyote.Kwanza wanaheshimu kazi yao kwa kufanya kwa utulivu.Yaani myansa hata kama humpendi kuna mafunzo utapata au muulize yule rafiki yangu kule Landani alipofika akaduwaa kwa nyodo,lakini akaona kuna jipya kwa wanyasa,mwishowe akatoa heshima zote kama askari jeshini,upo?tazama kwa hamu samaki haji bure huko mjini kwenu wavivu wakubwa .....aaaah samahani natania....unanichukia mimi myn asa?aah!lakini ...ebuu ngoja kwanza.Sawa...ngoja nikomee hapa.

1 comment:

  1. Basi ngoja nami nije huku na nianza kazi ya kuvua au labda niwe mchuuzi.

    ReplyDelete

Maoni yako