July 02, 2008

Mnyasa Nimetua Mbinga Leo Unasemaje.......

Angalia picha hii kwa umakini halafu niambie inakupa fikra kidogo?Mmhh hapa ni barabara kuu ya Mbinga mjini pale,ukingalia kwa mbali kidogo kuna jengo au mnara fulani-hapo ni jimboni au makao makuu ya jimbo la mbinga.Sasa itazame barabara hii halafu jiulize ni mara ngapi unapenda hali hiyo,ni namna gani unaweza kuwa na ustadi wa mazingira bora au maisha bora kwa kila raia.Lakini sitaki ulaumu ila nimependa sana hii picha nilipoipiga kwa mara ya kwanza kwani inaonyesha njia kuu ya mjini na maduka pembeni.Ukiwa upande wa juu pale karibu na hoteli ya Madina njia panda ya benki ya NMB na barabara ya kwenda kiwanda cha kahawa ndipo barabara hii ilipo.Ni barabara kuu katikati ya mji.Habari ndiyo hiyooo wabunge wa jimbo la Mbinga magharibi na mashariki.

1 comment:

  1. Asante ndugu.

    Umenikumbuschia nyumbani.

    Cheers,
    Dan

    ReplyDelete

Maoni yako