March 08, 2010

NIMEIBUKIA WAPIIIIIIIIIII JAMANIIIIIII?

Kwa watu wangu woteeeeeeeeeeeeeeee hamyambu yambu jamani kanonooooooo??? Unajua nimeibukia wapiiii? Hebu angali hilo lipicha unadhani nipooo? Thubutu ukiweza nakupa zawadi niliyopata Makumbusho yao hapa.

KIFUPI
Nimeibukia BAGA-HEART a.k.a Bagamoyo nimezungunga mitaani kama chokoraa tangu kumekucha na muda ninaopata ni huu kuandika baada ya MICHAKATO kibaoo inayohusu.

Nipo najaribu kuanglia namna ninavyoweza kuibadilisha akili yangu na kujiangalia zaidi huku nikiambatana na rafiki zangu wenye hamu ya kujua sisi waafrika tupoje na majengo yetu ya kale yapoje, nyoooo. Si vibaya, ila nashukuru kuwa anaongeza kipato kwa serikali yetu adhimu duh!
Bagamoyo kwa upendo wa kuwaonyesha hawa wenye rangi za albino a.k.a washamba(natania, maana ananingalia huyu hapa) maana wakiona mishale na mikuki wanaduwaa meno 32 nje kama wamefumaniwa.... Lol ipo kazi
Si wamezoea kuona mibunduki ya akina Joji Kichaka.
Haya tazameni hiyo picha basii oneni wenyewe

1 comment:

Maoni yako