May 31, 2010

PENDEKEZO LA WASTANI LA MFUMO MFUMO WETU WA UTAWALA

Pendekezo la wastani la mfumo wetu wa utawala.

Na Markus Honorius Mpangala, Mbinga-Ruvuma

Msingi mkubwa wa kujitawala ni maamuzi ambao yanasimamia madhumuni yaliyomo katika makabrasha yetu. Maamuzi haya yanawalenga watu wetu waliomo bila kujari kabila,nasaba na uenyeji wao. Ilimradi walengwa ni raia halali wa Tanzania.

Ziko njia nyingi za maamuzi ambayo humaanisha muundo wa utawala. Njia hizi hushirikisha pamoja kati ya wananchi,serikali yao na wawakilisha wa majimbo,kata na kadhalika. Mfumo huu unajikitia kuonyesha kuwa taifa letu linaoubunifu wake kiutawala.

Tunaweza kuunda mifumo mipya au kuikarabati ile ya zamani katika ngazi za mikoa,wilaya,tarafa, kata na vijiji. Maeneo haya ndiyo huunda taifa ambalo leo tunajivunia na kujiita Watanzania wenye Jamhuri ya Tanzania.
Usipitwe Isome

1 comment:

Maoni yako