October 17, 2012

HARAKATI ZA MAENDELEO WILAYA YA NYASA, KARIBU KUWEKEZA


Wilaya ya Nyasa ni miongoni mwa Wilaya mpya zilizoanzishwa na serikali ya awamu ya nne. Habari za kuundwa wilaya ya Nyasa nilianza kuzisikia mwaka 1993 nikiwa shule ya msingi. Lakini mwaka huu Wilaya ya Nyasa imezinduliwa rasmi na shughuli za maendeleo zinaendelea ili kukidhi mahitaji ya wananchi. Katika harakati hizo ni pamoja na huduma ya Maji ambayo ni muhimu sana kwa wananchi wa Wilaya hiyo. Hapa ni picha mbalimbali ambazo zinaonyesha suala la upatikanaji wa maji katika vijiji mbalimbali wilayani humu.  Bila shaka wageni na wenyeji watavutiwa kuwekeza katika wilaya mpya ambayo fursa mbalimbali zinajitokeza. karibuni. Picha zote na Hoops Kamanga
 Chanzo cha Mradi wa maji kikifanyiwa ukaguzi.
 Tenki la Maji katika mradi wa maji katika kijiji cha Ng'ombo wilaya ya Nyasa
 Mradi wa Maji katika kijiji cha Kindimba Juu ambao umekamilika na wananchi wanategemea kutumia siku chache zijazo. Hapo fundi anamalizia marekebisho katika tenki.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako