November 07, 2012

UJENZI WA MACHINJIO MBINGA NA SOKO LIWETA


Katika kuboresha huduma za jamii, kuna mengi huwa yanafanyika. Miongoni mwake ni kujenga Machinjio yenye ubora na mazingira salama kwa afya za wanadamu. Wilaya ya Mbainga imefanikiwa kujenga machinjio katika eneo la mbinga mjini. Machinjio hii itasaidia kuondokana na mazingira duni ya kuchinjia wanyama mbalimbali wanaopelekwa sokoni kuuzwa. Picha ya chini inaonyesha sehemu ya kusafishia utumbo katika Machinjio hayo mjini Mbinga.


Picha ya chini: eneo la Machinjio hayo, mjini Mbinga. Kama tulivyoeleza awali kuwa machinjio hii itawanufaisha sana wafanyabishara wa nyama na watumiaji kutokana na ubora uliopo, kulingana na kanuni za AFYA.

UJENZI WA SOKO
Ujenzi wa Soko la Kijiji cha Liweta. Ujenzi huo upo katika awamu ya kwanza. Unatarajiwa kukamilika mapema mwakani ili kuhakikisha wakazi wa kijiji hicho wanaweza kuwa na Soko lenye kiwango kizuri baada ya kutokuwepo kwa Soko kwa muda mrefu. ni njia moja wapo ya kuweka mazingira safi na kuwawezesha wauzaji wadogowadogo kuuza bidhaa zao katika mazingira mazuri.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako