January 24, 2013

HAPPY BIRTHDAY CHADEMA


Ben Saaanane

Na Ben Saanane, Dar es Salaam
Hebu tuone:Chama cha Patriotic Front cha Zambia(Ninakifananisha na CHADEMA katika Historia na Harakati zake Kuchukua Dola) kilichoanzishwa Mwaka 2001 kimeweza kuwa chama imara kwa kuwachukulia hatua wasaliti bila kujali cheo au nafasi ya mtu.
Leo hii tunapoandika hapa waziri wa mambo ya nje Given Lubinda anajiandaa kukutana na kamati ya Nidhamu ya chama hicho kwa tuhuma za kukisaliti chama hicho na kushirikiana na vyama hasimu.
Akipatikana na hatia kwenye kamati kuu ya PF atafukuzwa uanachama moja kwa moja.
Pia wakati huo huo kiongozi wa upinzani Hakainde Hichilema wa chama cha UPND(nilishawahi kukifananisha na chama cha CUF) anakabiliwa na mashtaka ya defamation huku chama Tawala cha Zamani cha MMD(CCM ya Zambia iliyounda aliiance na UPND kuihujumu PF) kikipambana kujinusuru kisifutwe kwa kukiuka sheria na kuhodhi mali za umma.Huu ni mfano mzuri wa kufuata misingi na sio kufuata watu.
Hakuna aliyewahi kuwa juu ya chama.Chama cha ODM nchini Kenya kilichoanzishwa mwaka 2005 kilionyesha njia kuwaondoa akina Ruto,Chama cha MDC nchini Zimbabwe kilichoanzishwa mwaka 1999 kilionyesha njia kwa kuwaacha akina prof.Arthur Mutambara,CCM Chini ya uenyekiti wa Mwl.Nyerere kilifuata Misingi kwa kumfukuza Maalimu Seif akiwa waziri kiongozi(NASIZITIZA CCM ya NYERERE)....CHADEMA leo kimefikisha miaka 20 Rasmi tangu kisajiliwe.
Tuendelee kufuata misingi kwa mifano hii.Happy Birthday CHADEMA,Viva M4C

No comments:

Post a Comment

Maoni yako