January 24, 2013

JOHN STEVEN AKHWARI ANASTAHILI HESHIMA


Na Hance Forogo, Dar es salaam
Mzee wetu tunayempa Heshima leo alizaliwa mwaka 1938 katika wilaya ya Mbulu iliyoko mkoa wa Arusha....hapa namzungumzia mzee John Steven Akhwari!....akiwa kijana mdogo kabisa alianza kujiingiza katika mchezo wa riadha na haikumchukua muda mrefu kuwa mwanariadha wa mbio ndefu wa kutegemewa na Taifa la Tanzania akishiriki mashindano mengi ndani na nje ya Tanzania na amewahi kuwa bingwa wa mbio ndefu wa bara la Afrika,pia mwaka 1970 alimaliza mbio akiwa na 05 katika mashindano ya mbio ndefu kwa nchi za jumuia ya madola!....
Akitumia muda wa 2:15:05 wakati mshindi alitumia muda wa 2:09:28,inaaminika kuwa alikuwa ni mkimbiaji "World Class" mwenye hadhi ya dunia kati ya miaka ya 1960 na 1980!....
Katika tukio la kihistoria,mzee Akhwari katika mashindano ya Olimpiki mwaka 1938 nchini Mexico,katika mji wa Mexico akiwa wanafanya utani na wakimbiaji wa kuviziana na wakimbiaji wengine ili kupitana na kuwania ushindi alianguka ghafla akiwa amemaliza 19km kati ya 42km.
Baada ya kubanwa na misuli tatizo lililotokana na hali ya hewa kwani kabla hakuwa amefanya mazoezi katika mazingira yenye hali ya miinuko na hali ya nchi kama ya Mexico.
Kutokana na tukio hilo aliteguka goti na kupata jeraha kubwa pia alipata maumivu makali kwenye bega lake!.....hata hivyo aliendelea na mashindano na kumaliza wa mwisho akitumia muda wa 3:25:27 kati ya 57 waliomaliza mbio wakati wanariadha 18 hawakuweza kumaliza mbio huku mshindi Mamo Wolde toka Ethiopia akitumia muda wa 2:20:26!....baada ya muda mfupi kumaliza mbio zake,waandishi walimfuata na kumuuliza kwa nini aliendelea na mbio wakati alikuwa ameumia sana!?....
akajibu kuwa "Nchi yangu(Tanzania) haikunituma kushiriki maili 5000,imenituma nije kumaliza mbio za maili 5000" Jina lake linatumiwa na taasisi ya John Steven Akhwari Athletic Foundation ambayo inatumika kuandaa wanamichezo wanaojiandaa kwa mashindano ya Olimpiki,mwaka 2000 alialikwa kwenye mashindano ya Olimpiki yaliyofanyika Sydney nchini Australia na baada ya hapo alichaguliwa kuwa balozi wa heshima katika maandalizi ya mashindano ya Olimpiki jijini Beijing,China,pia 13/04/2008 alihusika na ubebaji wa Mwenge wa Olimpiki ulipokuja Tanzania katika maandalizi ya Olimpiki!....
Licha ya kwamba mwaka 1983 mzee wetu alitunukiwa medal ya heshima kama shujaa wa Taifa "National Hero Medal of Honor" hatuna budi nasi pande hizi KUMPA HESHIMA ZAKE kwa juhudi kubwa na uzalendo alioufanya kwa ajili ya nchi yake!....ameitangaza nchi kupitia mchezo wa riadha!.....
Huyo ndiye mzee John Steven Akhwari ambaye kwa sasa ni mkulima stadi,hakika anastahili HESHIMA!....Thanx!...

No comments:

Post a Comment

Maoni yako