January 11, 2013

NIDHAMU YA WALIMU WETU KAMA WANAMUZIKI WA BONGOFLEVA


Na John Chitanya, Nyasa
Naandika baada ya kufanya ziara fupi kutembelea shule ya sekondari ya Monica Mbega iliyopo Kata ya Mbaha katika Tarafa ya Ruhuhu. Nilianza safari yangu katka kijiji cha Lundu kuelekea Mbaha, ambapo umbali wake ni kilimita 1, niliwasili shuleni hapo yapata saa asubuhi.
Lengo la safari hiyo ni sehemu ya mkakati wa kutembelea shule zote za Kata katika Tarafa ya Ruhuhu, kisha shule za Tarafa ya Ruhekei kwenye wilaya mpya ya Nyasa. Nilipowasili shule hapo nilikusudia kuangalia mazingira ya shule na namna gani walimu wa shule hiyo wanavyowasilia katika uwajibikaji wao kwa wanafunzi na namna gani wanafunzi wanawajibika kwa walimu wao ili kujenga nidhamu na mafanikio ya shule.
Nidhamu baina ya mwalimu na mwanafunzi ndio msingi mkuu wa kulefa mafanikio ya shule yoyote.
Mpaka naondoka shuleni hapo saa moja na nusu sikufanikiwa kumuona mwalimu yeyote hata wa zamu hakuwepo, mazingira ya wanafunzi nao wapo kama wapo msibani hakuna shughuli za usafi wa mazingira. Nilijaribu kumhoji mmoja wa wanafunzi kama wamefanya ‘roll call’, nikaambiwa muda bado haujafika. Wakati huo ilikuwa saa moja na robo. Mpaka muda huo nilikuwa na wanafunzi wasiozidi 50.
Wanafunzi wa shule ya msingi Mango, wilayani Nyasa. 
Picha kwa Hisani ya Tanzglo
Na kati yao hapakuwa na mwenye saa. Picha hiyo unatarajia patakuwa na hali nzuri kimasomo, wajibu na nidhamu kati ya mwalimu na mwanafunzi? Kwahiyo hali nzuri ya kitaaluma kwa shule kama hiyo sio jambo linaloweza kutokea, kwa vile mwanafunzi hurithi tabia za wakubwa naamini wanafunzi watakuwa katika hali gani kitabia na kitaaluma toka kwa walimu hao? Kama mwalimu ni mvivu kuwahi shule unatarajia atapanda mbegu gani kwa wanafunzi wake? Nilipojaribu kutaka kujua kama walimu wanakaa mbali na maeneo ya shule niliambiwa wote wanakaa ndani  ya mita 100 toka shuleni hapo. Je unatarajia nini kwa shule kama hiyo?
Nilifanya ziara hiyo kwakuwa mwezi wa pili nilikuwa katika kikao cha tathmini ya matokeo ya mitihani ya taifa kwa kidato cha pili na nne. Nilienda kwa niaba ya mzee kwa wanafunzi. Katika matokeo ya kidato cha pili walikuwa wanafunzi sio chini ya 47, lakini waliovuka wastani ni wanafunzi watatu tu. Katika matokeo ya kidato cha nne hawakuzidi wanafunzi 37, lakini waliopata vyeti kwa daraja la nne kwa pointi  29-33 ni wanafunzi 6 pekee na wanafunzi waliobaki walifeli.
Wakati ule mkuu wa shule alijitetea kwenye kikao cha tathmini kuwa shule haikuwa na walimu  wa kutosha kwani walikuwa watatu tu. Kwa sasa shule hiyo ina walimu 8 bado hawatoshi. Kama walimu 8 hawafiki darasani kwa muda mwafaka wakiwa walimu 20 itakuwaje hali ya shule hiyo? Sitakosea nikisema walimu hao ipo siku watafika shuleni saa sita mchana kwa kufuata muda wa vipindi vyao tu? Leo nimekumbuka msemo wa walimu  wa siku hizi  ni walimu wa bongofleva wanafika shuleni wamevaa suluali za jeans. Na wao wanajitetea kuwa ualimu sasa sio wito bali kazi, na kama wito ulikuwa zamani sana. Sijui, natafakari tu.

•    John Chitanya, ni mwandishi na mwalimu wa Miracle Center iliyopo Songea. Maoni: 0718 005557

1 comment:

Maoni yako