December 19, 2013

NYASA NA MATAMANIO YA UJENZI WA NYUMBA ZA KITALII


Na Vitus Matembo, Ndengele
Ukanda wa ziwa Nyasa huvutia sana hasa kutokana na mandhari yake kuwa ya kustaajabisha machoni kwa wageni. Hali ambayo inatarajiwa kuongezeka zaidi miaka ijayo kutokana na kasi iliyopo.
Lakini jambo kubwa zaidi ni ujio wa wageni hususani wazungu umeleta chachu ya uwekezezaji na maendeleo ya kijamii na uchumi.
Hoteli ya Mbunge wa Jimbo la Mbinga Magharibi(Nyasa), John Komba.
Nyumba iliyojengwa juu ya Jiwe katika kijiji cha Ndengele.
Katika suala la ujenzi wa nyumba, kwa muda sasa nimeshuhudia mzungu mmoja akijitahidi kujenga Nyumba ya Ghorofa Juu ya jiwe. Alianza muda mrefu ila mwaka huu ameikamilisha Kwakweli inavutia sana.  Nyumba hiyo ipo katika kijiji cha Ndengele, Wilayani Nyasa, kando kando ya barabara itokayo MBAMBA BAY kwenda LIULI.
Wengi wameshangazwa na ujenzi huo kuwa kwanini ajenge juu ya jiwe. Ila kwangu binafsi naona haina tatizo na nyumba ni nzuri sana.
Natamani nipate nafasi ya kuishi kwenye nyumba kama hiyo kwani Mandhari ya ziwa Nyasa huonekana vyema sana hususani fukwe ya Mbamba bay na Ghuba yake yote.

Aidha, Mbunge wetu, Mh. JOHN KOMBA naye ameamua kujenga hoteli yake pembezoni mwa ziwa hapa mjini Mbamba bay, wilayani Nyasa. Huu ni mwanzo tu wa kupeperusha utalii wa Nyasa. Mengi yatawajia, Usikose kutembelea mara kwa mara blog yetu upate uhondo.

KARIBUNI NYASA WAPENDWA WETU

1 comment:

  1. Ndengele ...ninekumbuka mbali sana ..ni kijiji cha kwanza toka Lundo...lwika au ni Chinula?.....

    ReplyDelete

Maoni yako