December 19, 2013

KINACHONIKERA KATIKA WILAYA YANGU YA NYASA


Na Vitus Matembo, Mbamba Bay
Nyasa ndio Nyumbani halisi, nimezaliwa na kukulia katika mji wa Mbamba bay. Pia nimewahi kuishi vijiji vingi ukanda wa ziwa Nyasa kama vile Mkali, Ndengele, Mtipwili, Lundo, Kilosa na Ndesule kutokana na kuhamishwa kikazi kwa Mzazi wangu ambaye ni mwalimu.
Nimewahi kutembelea vijiji vingne kama vile Mango, Tumbi, Kihagara na Ng'ombo Ila kwakweli Jiografia ya Nyasa ni nzuri ukiitafakari kwa kina. Kwa wageni huwa ni lulu wafikapo Nyasa. Kwa muda wote huo bado nimeendelea kuipenda Nyasa yangu ila toka utotoni kitu UCHAWI imekuwa kero sana katika masikioni mwangu.
Uchawi ndio changamoto inayoleta kuoneana wivu katika maendeleo na ndicho kinachorudisha maendeleo hapa kwetu Nyasa. Mtu akisoma sana/ akiwa na akili sana lazima achezewe au kufanyiwa mambo ya kichawi. Kwa mfano mimi napata tabu sana kwa kupigwa chale karibu kila wiki. Hakika naumia sana, japo sina namna kwani ndiyo Nyumbani.
 
Wengne huwa hawaji Nyasa kabisa hata kama ni kwao, ila kwangu nitavumilia tu na nimebakia kumuomba Mungu ili aniepushe ni hao waovu. Kwa mfano toka nimalize chuo mwezi june mwaka huu. Nilipofika Nyasa nimesikia na kuona matukio mengi ya kutatanisha kama vile kukuta nyama ya binadamu sebuleni huko kijijini Chiulu. Pia babu kumlazimisha mwanae aende ziwani na kusababsha kifo. Vilevile askari waliotoka Depo kufa maji kiholela. Matumizi ya radi kuuana.

Kubwa kabisa na la kustaajabisha ni uwepo wa mamba wa watu ziwani. Kwa mfano mwezi uliopita kuna mamba aliuawa alipopasuliwa tumbni watu hawakuona Nyongo, si kwamba ilipasuka LAHASHA, ila haikuwepo.(ona pichani). 
HAKIKA KWA MATUKIO YA UTATA KAMA HAYA YANANIPA CHANGAMOTO KUBWA.
Ila haina maana ya kukukimbia Nyasa ndo suluhisho, hapana ila kinachotakiwa ni kuzidi kutoa elimu kwa jamii ili kutokomeza imani za kishirikina.
MABADILIKO DAIMA HUANZA NA WEWE.

"PAMOJA TUIJENGE NYASA"

No comments:

Post a Comment

Maoni yako