September 14, 2017

MAMBO 10 ALIYOSEMA RAILA ODINGA BAADA YA KUSHINDA KESI



Mara baada ya Jaji wa Mahakama ya Juu kutangaza kufuta matokeo ya uchaguzi, Raila Odinga alizungumza na vyombo vya habari na kueleza mambo yafuatayo.
1.Aliishukuru Mahakama ya Juu kwa kuzingatia sheria na kubatilisha matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 8 mwaka huu.
2. Alitoa shukrani kwa Majaji wawili walipinga kurudiwa uchaguzi huo, Jaji Njoki Ndungu na Jaji JB Ojwang kwasababu walisimamia wanachokiamini.
3. Amethibitisha kuwa Tume ya uchaguzi IEBC imekuwa ikikiuka kanuni na taratibu za uchaguzi wakati wa kuhesabu kura za urais.
4. Baada ya ushindi, Raila alikwenda kuipongeza timu ya Mawakili wake James Orengo (Seneta wa Siaya ) na Otiende Omollo.
5. Nafasi ya waangalizi wa kimataifa wa uchaguzi inatakiwa kuwekewa mtazamo mpya kwasababu wanaweza kuhongwa.
6. Waangalizi wa kimataifa waliokuwa bega kwa bega na NASA wameuangusha upinzani nchini humo na walikuwa na lengo la kutafuta umaarufu tu.
7. Kuna umuhimu na kila sababu ya kuangalia nani atakuwa msimamizi wa uchaguzi wa marudio utakaofanyika ndani ya siku 60 baada ya hukumu ya mahakama.
8. Amependekeza Makamishna na maofisa wa Tume ya uchaguzi IEBC na Mkurugenzi mtendaji wanapaswa kushtakiwa.
9. Ni muhimu kufanya ukaguzi katika mifumo ya mawasiliano ya Tume ya IEBC.
10. NASA inatarajia kuona mabadiliko katika uchaguzi ujao.

©Nishani Media,
Dar es salaam
4/9/2017

No comments:

Post a Comment

Maoni yako