September 21, 2017

SERIKALI IMEKATA RUFAA KATIKA KESI ILIYOSHINDWA YA UMRI WA MTOTO WA KIKE KUOELEWA



DAR: Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Kupitia ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali imekata rufaa kesi iliyoshindwa mwaka Jana Baada ya Rebecca Gyumi Mkurugenzi wa Taasisi ya Msichana Initiative kufungua kesi ya Kupinga Ndoa za umri mdogo.

Sheria ya Ndoa ya Mwaka 1971 inaruhusu mtoto wa kike kuelewa akiwa na miaka 14. Rebecca Gyumi alifungua kesi hiyo Mwaka Jana kupiga sheria hii Kandamizi dhidi ya watoto wa kike walio chini ya umri wa miaka 18 kuolewa kwani wanakosa fursa ya kupata elimu

Mwaka jana Mahakama Kuu ilitoa amri Kwamba Serikali ipeleke mswaada Bungeni kuondoa sheria hiyo, Kinyume chake Serikali imefungua rufaa kupinga Uamuzi huo ikitaka sheria hiyo iendelee kuwepo ili watoto wenye umri chini ya miaka 18 waolewe kama wenye zaidi ya miaka 18

Ndimi,
Ndahani N. Mwenda

No comments:

Post a Comment

Maoni yako