September 22, 2017

BASI LA KISUMAPAI LAPATA AJALI NANGOMBO





Basi la kampuni ya Kisumapai lenye namba za usajili T 606 CTY   linalofanya safari zake  kutoka Songea kwenda Mbamba Bay, Liuli hadi Mango wilayani Nyasa limepata ajali mapema leo katika kijiji cha Nangombo wakati likitokea Songea kuelekea Mbamba Bay.
Taarifa inasema kuwa abiria wanne wamefariki dunia kutokana na ajali hiyo, huku wengine wakiwa wamejeruhiwa na kukimbizwa katika hospitali ya Mbamba Bay.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako