November 03, 2017

WATU WASIOFAHAMIA WAMPIGA MAWE MTU HADI KUFA


NA MWANDISHI WETU

MTU mmoja aliyetambulika kwa jina la Gaudansi Kapinga(31) aliyekuwa Mkazi wa Kijiji cha Mbuyule Tarafa ya Ruhekei wilayani Nyasa mkoani Ruvuma,ameuawa kwa kupigwa na mawe hadi kufa na wananchi wa kijiji hicho.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma SACP Gemini Mushi (pichani) amesema tukio lilitokea Novemba 2,2017,majira ya saa mbili usiku katika kijiji hicho ambapo watu wasiofahamika walijichukulia sheria mkononi na kumua marehemu huyo.


Kamanda Mushy amebainisha kuwa inadaiwa katika tukio hilo,marehemu anadaiwa kukutwa akivunja duka la Furaha Matembo na kwamba upelelezi wa kina unaendelea kufanywa na Jeshi la polisi pamoja na kuwasaka watuhumiwa wa tukio hilo.

Katika tukio jingine lililotokea jana majira ya saa nne usiku,Kamanda Mushi  amesema Jeshi la Polisi limewakamata watu saba katika Mtaa wa Misufini wilayani Tunduru wakiwa na kiasi cha lita sita za pombe haramu aina ya gongo.

Kamanda Mushi anatoa raia kwa wananchi wa Mkoa wa Ruvuma kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi,badala yake wawafikishe watuhumiwa katika vyombo vya sheria na kwamba waache biashara haramu ya gongo kwa sababu serikali itawachukulia hatua za kisheria.

©Songea Municipal, Ruvuma. 

HIVI PUNDE…
Thomas Chihongaki anasema, “Gaudansi Kapinga sio Mkazi wa Kijiji cha Mbuyula bali hao Vijana walikuwa wageni kabisa hapo Kijijini mwenzie Kakimbia,”.

No comments:

Post a Comment

Maoni yako